Pages

Friday, 13 April 2012

Ukweli Barani

Nchi ya Chad ndio ya pili duniani ambayo Uchumi wake unakuwa kwa kasi.

Winnie Madikizela-Mandela




Winnie Mandela alizaliwa Nomzamo Winfreda Madikizela tarehe 26 Septemba 1936, ni mwanasiasa kutoka Afrika ya Kusini na alishikilia nyadhifa mbalimbali serikalini na pia alikiongoza African National Congress ya Wanawake. Hivi sasa ni mwanachama wa ANC Kamati Kuu ya Taifa.Ingawa bado alikuwa ameoleka na Nelson Mandela wakati alikuwa rais wa Afrika Kusini mnamo Mei 1994,wanandoa hawa walikuwa wametengana miaka miwili baadaye. Talaka yao ilimaliza 19 Machi 1996, na makazi isiyojulikana nje ya mahakama. Jaribio la Winnie Mandela kupata makazi ya hadi dola milioni 5, nusu ya yale alidai ni thamani ya mume wake wa zamani, yalitupiliwa mbali na mahakama kwa kutoonekana mahakamani.
Ni mwanaharakati matata, ni maarufu miongoni mwa wafuasi wake, ambao humuita ''Mama wa Taifa'' hasa kutokana na ushiriki wake katika madai ya ukiukaji haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na utekaji nyara wa 1988 ambapo mwanaharakati mmoja wa miaka 14 wa chama cha ANC Stompie Moeketsi aliuawawa.
Machi 2009 tume ya Uchaguzi ilitoa uamuzi kuwa Winnie Mandela ambaye alichaguliwa kama mgombea wa ANC, anaweza kuwania Uchaguzi mkuu wa Aprili 2009, licha ya kuwa na kesi kotini na udanganyifu.
Jina lake Nomzamo linalomaanisha ''ajaribuye kitu'', alikutana na wakili na pia mwanaharakati Nelson Mandela 1957, Walioona 1958 na wana wasichana wawili. Juni 2010 alitibiwa kwa mshutuko wa moyo baada ya kusikia mjuku wake amefariki kwa ajali ya barabara usiku wa kufungua Kombe la Dunia. Ana ugonjwa wa Kisukari.
Licha ya vikwazo vya elimu kwa watu weusi wakati wa ubaguzi wa rangi,alipata shahada katika kazi za kijamii kutoka Jan Hofmeyer huko Johannesburg.
Bi. Mandela alijitokeza kama mpinzani kiongozi kwa wazungu wachache waliokuwa utawalani wa serikali katika miaka ya kifungu cha mumewe toka Agosti 1963 – Februari 1990, katika miaka hii alikuwa akikimbilia uhamishoni Brandfort isipokuwa ile tu siku aliyokubaliwa kumtembelea mumewe katika gereza la Roben Island.
Sifa yake iliharibika wakati akitoa hotuba yake Aprili 13 1986 wakati alitetea na kukubali watu kuchomwa wakiwa hai wakitumia gurudumu za gari ili kumaliza ubaguzi wa rangi. Fauka ya hayo hathi yake iliendelea kuharibika pale mlinzi wake, Jerry Musivuzi Richardson alisema eti Winnie aliamurisha utekaji nyara na mauaji.Desemba 29 1988 Richardson ambaye alikuwa kocha wa klabu ya mpira ya Mandela United ambayo ndiyo ndiyo ilikuwa kama ulinzi wa kibinafsi wa Bi. Mandela alisema kwamba ndiye aliyemuuwa kijana wa miaka 14 James Seipei ama Stompie Moeketsi miongoni mwa vijana wengine watatu.

Vituko

Mwanamke mmoja ampiga mmewe kisa na maana alipokuwa akienda kitandani wakati wa kulala Mme wake hakuenda kitandani naye bali alibaki aki facebook.

Thursday, 12 April 2012

Joyce Banda



Ni mwanasiasa kutoka malawi ambaye pia amekuwa rais nchini humo tangu Aprili 7 2012.Msomi na mwanaharakati, alikuwa waziri wa nchi za kigeni toka 2006 hadi 2009 na Makamu wa Rais wa nchi hiyo tangu Mai 2009 hado Aprili 1012. Alikuwa rais kutokana na kifo cha gafla cha Bingu wa Mutharika. Ni mwanamke wa kwanza kuwa rais na makamu wa rais nchni Malawi.
Alikuwa pia mbunge na waziri wa jinsia, watoto na mambo ya Huduma za jamii. Kabla ya kushiriki katika siasa alikuwa mwanzilishi wa Joyce Banda Foundation, Mwanzilishi wa Chama cha Taifa cha Wafanyi biashara Wanawake (NABW), Viongozi Wanawake wachanga na mtandao wa mradi wa njaa. Alitajwa katika Forbes Magazine 2011 kama mwanamke wa tatu maarufu na mwenye nguvu zaidi katika Afrika.
Alikuwa mwanzilishi na mwenyekiti wa chama cha People's Party kilichoundwa 2011, na kabla ya kifo cha rais Mutharika alikuwa awanie urais wa nchi hiyo mwaka 2014. Banda anatoka Malemia, kijiji katika Wilaya ya Zomba ya Malawi. Ana Certificate kutoka Chuo cha Cambridge School na shahada ya sanaa katika Elimu ya Mafunzo kutoka Chuo Kikuu cha Columbus na stashahada katika usimamizi yaani (Management) aliyopata nchini Italia.
Katika umri wa miaka 25 alikuwa tayari kashapata watoto watatu na alikuwa anaishi Nairobi Kenya. Yeye ni dada kwa Anjimile Oponyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Academy ya wasichana iliyoanzishwa na mwimbaji Madonna.
Ameolewa na Richard Banda,aliyekuwa Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Malawi.
Ana zawadi zaidi ya 10 kutoka nchini malawi na kimataifa.



Vituko

Mtoto mwenye umri wa miaka 15 ameokolewa na mwa wa jirani wao, baada ya kukimbizwa na kahaba mwanamke aliyekuwa anamdai. Mtoto huyo alikuwa anatoka dukani alipokuwa ametumwa na mamaye mwendo wa saa kumi na mbili jioni, hapo ndipo mwanamke huyo alipomuona na kuanza kumkimbiza, ndipo mbwa wa jirani alipomuona na kuanza kumkimbiza mwanamke huyo.

Ukweli Barani

Libreville, Gabon ndio nchi ya 5 Duniani ya gharama ya juu ama kubwa kuishi. Tokyo ndio ya kwanza.

Wednesday, 11 April 2012

Steven Kanumba


Steven Charles Kanumba alikuwa msanii wa maigizo na filamu kutoka nchini Tanzania. Katika historia ya tasnia ya filamu nchini Tanzania, Kanumba ndiye aliyekuwa msanii wa kwanza nchini kufanya kazi nje ya nchi na kuweza kuwavuta wageni kutoka nchi mbalimbali kuja kuigiza Tanzania. Hasa walikuwa Wanigeria kama vile Mercy Johnson, Emmanuel France, Nkiru Silvanus, Ramsey Nouah, na wengine wengi tu. Kanumba pia ameweza kuwaleta waongozaji filamu kadhaa was Kinigeria nchini.




Steven alizaliwa huko Shinyanga Januari 8 1984, alianza masomo yake katika shule ya msingi ya Bugoyi, na kuendela na masomo ya sekondari huko Mwadui na baadae kupata uhamisho katika shule moja jijini Dar es Salaam iitwayo Dar Christian Seminary. Alivyomaliza kidato cha nne akaendelea na masomo ya kidato cha tano na sita katika shule ya sekondari ya Jitegemee ilioko huko huko Dar es salaam.
Kanumba alieanza shughuli za kuigiza miaka mingi kwenye miaka ya "90". Ila kufahamika zaidi alianza mwaka 2002 mara tu baada ya kujiunga na kundi la sanaa ya maigizo maarufu kamaKaole Sanaa Group.

Hivi sasa amejibebea umaarufu mkubwa nchini Tanzania na amekuwa kipenzi cha wengi na amekubalika karibuni nchi zote za Afrika Mashariki na maziwa makuu.
Kwa sasa ameanza kutangaza sanaa nchi za Afrika ya Magharibi ikiwemo Nigeria na pia Wanigeria wamependezewa na uigizaji wake hivyo kushirikiana pamoja naye katika filamu kadha wa kadha. Filamu ambazo wameshawahi kushirikiana pamoja ikiwemo na ile ya Dar to Lagos, She is My Sister na nyingine ambazo bado zinajengwa.
Steven Kanumba alitangaza hivi karibuni nia ya kuwa mgombea katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015. Aliaga dunia tarehe 7 Aprili, 2012) na kuzikwa hapo jana ma mia ya waombolezaji wakiwemo watu mashuhuri serikalini pamoja na Mama Salma Kikwetu walihudhuria na kumuaga.