Pages

Thursday, 12 April 2012

Joyce Banda



Ni mwanasiasa kutoka malawi ambaye pia amekuwa rais nchini humo tangu Aprili 7 2012.Msomi na mwanaharakati, alikuwa waziri wa nchi za kigeni toka 2006 hadi 2009 na Makamu wa Rais wa nchi hiyo tangu Mai 2009 hado Aprili 1012. Alikuwa rais kutokana na kifo cha gafla cha Bingu wa Mutharika. Ni mwanamke wa kwanza kuwa rais na makamu wa rais nchni Malawi.
Alikuwa pia mbunge na waziri wa jinsia, watoto na mambo ya Huduma za jamii. Kabla ya kushiriki katika siasa alikuwa mwanzilishi wa Joyce Banda Foundation, Mwanzilishi wa Chama cha Taifa cha Wafanyi biashara Wanawake (NABW), Viongozi Wanawake wachanga na mtandao wa mradi wa njaa. Alitajwa katika Forbes Magazine 2011 kama mwanamke wa tatu maarufu na mwenye nguvu zaidi katika Afrika.
Alikuwa mwanzilishi na mwenyekiti wa chama cha People's Party kilichoundwa 2011, na kabla ya kifo cha rais Mutharika alikuwa awanie urais wa nchi hiyo mwaka 2014. Banda anatoka Malemia, kijiji katika Wilaya ya Zomba ya Malawi. Ana Certificate kutoka Chuo cha Cambridge School na shahada ya sanaa katika Elimu ya Mafunzo kutoka Chuo Kikuu cha Columbus na stashahada katika usimamizi yaani (Management) aliyopata nchini Italia.
Katika umri wa miaka 25 alikuwa tayari kashapata watoto watatu na alikuwa anaishi Nairobi Kenya. Yeye ni dada kwa Anjimile Oponyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Academy ya wasichana iliyoanzishwa na mwimbaji Madonna.
Ameolewa na Richard Banda,aliyekuwa Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Malawi.
Ana zawadi zaidi ya 10 kutoka nchini malawi na kimataifa.



No comments:

Post a Comment