Pages

Friday, 13 April 2012

Ukweli Barani

Nchi ya Chad ndio ya pili duniani ambayo Uchumi wake unakuwa kwa kasi.

Winnie Madikizela-Mandela




Winnie Mandela alizaliwa Nomzamo Winfreda Madikizela tarehe 26 Septemba 1936, ni mwanasiasa kutoka Afrika ya Kusini na alishikilia nyadhifa mbalimbali serikalini na pia alikiongoza African National Congress ya Wanawake. Hivi sasa ni mwanachama wa ANC Kamati Kuu ya Taifa.Ingawa bado alikuwa ameoleka na Nelson Mandela wakati alikuwa rais wa Afrika Kusini mnamo Mei 1994,wanandoa hawa walikuwa wametengana miaka miwili baadaye. Talaka yao ilimaliza 19 Machi 1996, na makazi isiyojulikana nje ya mahakama. Jaribio la Winnie Mandela kupata makazi ya hadi dola milioni 5, nusu ya yale alidai ni thamani ya mume wake wa zamani, yalitupiliwa mbali na mahakama kwa kutoonekana mahakamani.
Ni mwanaharakati matata, ni maarufu miongoni mwa wafuasi wake, ambao humuita ''Mama wa Taifa'' hasa kutokana na ushiriki wake katika madai ya ukiukaji haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na utekaji nyara wa 1988 ambapo mwanaharakati mmoja wa miaka 14 wa chama cha ANC Stompie Moeketsi aliuawawa.
Machi 2009 tume ya Uchaguzi ilitoa uamuzi kuwa Winnie Mandela ambaye alichaguliwa kama mgombea wa ANC, anaweza kuwania Uchaguzi mkuu wa Aprili 2009, licha ya kuwa na kesi kotini na udanganyifu.
Jina lake Nomzamo linalomaanisha ''ajaribuye kitu'', alikutana na wakili na pia mwanaharakati Nelson Mandela 1957, Walioona 1958 na wana wasichana wawili. Juni 2010 alitibiwa kwa mshutuko wa moyo baada ya kusikia mjuku wake amefariki kwa ajali ya barabara usiku wa kufungua Kombe la Dunia. Ana ugonjwa wa Kisukari.
Licha ya vikwazo vya elimu kwa watu weusi wakati wa ubaguzi wa rangi,alipata shahada katika kazi za kijamii kutoka Jan Hofmeyer huko Johannesburg.
Bi. Mandela alijitokeza kama mpinzani kiongozi kwa wazungu wachache waliokuwa utawalani wa serikali katika miaka ya kifungu cha mumewe toka Agosti 1963 – Februari 1990, katika miaka hii alikuwa akikimbilia uhamishoni Brandfort isipokuwa ile tu siku aliyokubaliwa kumtembelea mumewe katika gereza la Roben Island.
Sifa yake iliharibika wakati akitoa hotuba yake Aprili 13 1986 wakati alitetea na kukubali watu kuchomwa wakiwa hai wakitumia gurudumu za gari ili kumaliza ubaguzi wa rangi. Fauka ya hayo hathi yake iliendelea kuharibika pale mlinzi wake, Jerry Musivuzi Richardson alisema eti Winnie aliamurisha utekaji nyara na mauaji.Desemba 29 1988 Richardson ambaye alikuwa kocha wa klabu ya mpira ya Mandela United ambayo ndiyo ndiyo ilikuwa kama ulinzi wa kibinafsi wa Bi. Mandela alisema kwamba ndiye aliyemuuwa kijana wa miaka 14 James Seipei ama Stompie Moeketsi miongoni mwa vijana wengine watatu.

Vituko

Mwanamke mmoja ampiga mmewe kisa na maana alipokuwa akienda kitandani wakati wa kulala Mme wake hakuenda kitandani naye bali alibaki aki facebook.

Thursday, 12 April 2012

Joyce Banda



Ni mwanasiasa kutoka malawi ambaye pia amekuwa rais nchini humo tangu Aprili 7 2012.Msomi na mwanaharakati, alikuwa waziri wa nchi za kigeni toka 2006 hadi 2009 na Makamu wa Rais wa nchi hiyo tangu Mai 2009 hado Aprili 1012. Alikuwa rais kutokana na kifo cha gafla cha Bingu wa Mutharika. Ni mwanamke wa kwanza kuwa rais na makamu wa rais nchni Malawi.
Alikuwa pia mbunge na waziri wa jinsia, watoto na mambo ya Huduma za jamii. Kabla ya kushiriki katika siasa alikuwa mwanzilishi wa Joyce Banda Foundation, Mwanzilishi wa Chama cha Taifa cha Wafanyi biashara Wanawake (NABW), Viongozi Wanawake wachanga na mtandao wa mradi wa njaa. Alitajwa katika Forbes Magazine 2011 kama mwanamke wa tatu maarufu na mwenye nguvu zaidi katika Afrika.
Alikuwa mwanzilishi na mwenyekiti wa chama cha People's Party kilichoundwa 2011, na kabla ya kifo cha rais Mutharika alikuwa awanie urais wa nchi hiyo mwaka 2014. Banda anatoka Malemia, kijiji katika Wilaya ya Zomba ya Malawi. Ana Certificate kutoka Chuo cha Cambridge School na shahada ya sanaa katika Elimu ya Mafunzo kutoka Chuo Kikuu cha Columbus na stashahada katika usimamizi yaani (Management) aliyopata nchini Italia.
Katika umri wa miaka 25 alikuwa tayari kashapata watoto watatu na alikuwa anaishi Nairobi Kenya. Yeye ni dada kwa Anjimile Oponyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Academy ya wasichana iliyoanzishwa na mwimbaji Madonna.
Ameolewa na Richard Banda,aliyekuwa Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Malawi.
Ana zawadi zaidi ya 10 kutoka nchini malawi na kimataifa.



Vituko

Mtoto mwenye umri wa miaka 15 ameokolewa na mwa wa jirani wao, baada ya kukimbizwa na kahaba mwanamke aliyekuwa anamdai. Mtoto huyo alikuwa anatoka dukani alipokuwa ametumwa na mamaye mwendo wa saa kumi na mbili jioni, hapo ndipo mwanamke huyo alipomuona na kuanza kumkimbiza, ndipo mbwa wa jirani alipomuona na kuanza kumkimbiza mwanamke huyo.

Ukweli Barani

Libreville, Gabon ndio nchi ya 5 Duniani ya gharama ya juu ama kubwa kuishi. Tokyo ndio ya kwanza.

Wednesday, 11 April 2012

Steven Kanumba


Steven Charles Kanumba alikuwa msanii wa maigizo na filamu kutoka nchini Tanzania. Katika historia ya tasnia ya filamu nchini Tanzania, Kanumba ndiye aliyekuwa msanii wa kwanza nchini kufanya kazi nje ya nchi na kuweza kuwavuta wageni kutoka nchi mbalimbali kuja kuigiza Tanzania. Hasa walikuwa Wanigeria kama vile Mercy Johnson, Emmanuel France, Nkiru Silvanus, Ramsey Nouah, na wengine wengi tu. Kanumba pia ameweza kuwaleta waongozaji filamu kadhaa was Kinigeria nchini.




Steven alizaliwa huko Shinyanga Januari 8 1984, alianza masomo yake katika shule ya msingi ya Bugoyi, na kuendela na masomo ya sekondari huko Mwadui na baadae kupata uhamisho katika shule moja jijini Dar es Salaam iitwayo Dar Christian Seminary. Alivyomaliza kidato cha nne akaendelea na masomo ya kidato cha tano na sita katika shule ya sekondari ya Jitegemee ilioko huko huko Dar es salaam.
Kanumba alieanza shughuli za kuigiza miaka mingi kwenye miaka ya "90". Ila kufahamika zaidi alianza mwaka 2002 mara tu baada ya kujiunga na kundi la sanaa ya maigizo maarufu kamaKaole Sanaa Group.

Hivi sasa amejibebea umaarufu mkubwa nchini Tanzania na amekuwa kipenzi cha wengi na amekubalika karibuni nchi zote za Afrika Mashariki na maziwa makuu.
Kwa sasa ameanza kutangaza sanaa nchi za Afrika ya Magharibi ikiwemo Nigeria na pia Wanigeria wamependezewa na uigizaji wake hivyo kushirikiana pamoja naye katika filamu kadha wa kadha. Filamu ambazo wameshawahi kushirikiana pamoja ikiwemo na ile ya Dar to Lagos, She is My Sister na nyingine ambazo bado zinajengwa.
Steven Kanumba alitangaza hivi karibuni nia ya kuwa mgombea katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015. Aliaga dunia tarehe 7 Aprili, 2012) na kuzikwa hapo jana ma mia ya waombolezaji wakiwemo watu mashuhuri serikalini pamoja na Mama Salma Kikwetu walihudhuria na kumuaga.

VITUKO



Mwanamke mmoja afungwa miaka 10 gerezani kwa kumpa mtoto wake pombe aina ya vodka. Mtoto huyo mwenye umri wa miaka 5 alipatikana hajielewi na babake.Alipomuuliza mamake pia alikuwa amelewa chakari.  

UKWELI BARANI AFRIKA



Chura wakubwa zaidi duniani wanapatikana nchini Cameroon na ni zaidi ya futi moja.

Tuesday, 10 April 2012

Mohamed Amin



Mohamed ''Mo'' Amin alikuwa mpiga picha maarufu zaidi kutoka Kenya alithihirisha haya kwa picha na kanda zake za video alizopiga kuhusu njaa ya Ethiopia.Alizaliwa Agosti 29 1943, kwenye mtaa wa Eastleigh Nairobi na ari yake ya picha ilianza akiwa shuleni. Ndiye mwanzilishi wa kampuni ya Camerapix mwaka 1963 huko Dar es Salaam na kuihamisha kampuni hiyo hadi Nairobi.Katika miak ya 1970 akawa wapiga wa kutegemewa zaidi kuhusu habari za Afrika,akiripoti kuhusu vita na mapinduzi barani afrika na picha zake zilitumika pia na runinga na wanahabari wa magharibi
Ushawishi wake mkubwa ulikuja wakati picha zake pamoja Micheal Buerk mpiga picha mwenza ziliripotia Njaa ya Ethiopia zilipoleta hisia kimataifa na hatimaye kusaidiya na kusababisha matamasha ya Live Aid iliofanya wimbo ''We are the World'' wake wasanii wote ulimwenguni kutungwa.
Licha ya kujulisha ulimwengu kuhusu njaa ya Ethiopia alitoa na kupiga picha kumhusu Idi Amin na Mengistu Haile Mariam na pia ameandika vitabu kadha vikiwemo ''Journey Through Pakistan'' na zaidi ya hayo yote ameangazia kuhusu wanyama wa Afrika Mashariki na reli ya Uganda.
Novemba 23 1996 aliabiri ndege aina ya Ethiopian Airlines Flight 961 na Brian Tetley mwenye umri wa miaka 61 kurudi Nairobi baada ya kazi ya kibiashara nchini Ethiopia ndege hiyo ilitekwa nyara na kumlazimisha rubani kuilekeza ndege hiyo mashariki mwa bara indi, alijaribu kupigana nao watekanyara hao lakini ndege hiyo ikaaisha mafuta kuanguka kwenye ufuo wa visiwa vya Comoros. Amin aliaga papo hapo akiwa na umri wa miaka 53 rafikiye pia aliaga. 

VITUKO



Nusura harusi ikatizwe wakati Bi Harusi alipokiri kwamba alikuwa na mpango wa kando. Kulingana na walioshuhudia, mwanadada huyu alieleza kwamba atampenda mumewe hata ingawa anao mpango wa kando...!

FACTS



Maeneo kame kabisa duniani yanapatikana Afrika, nayo ni Al'Kufrah huko Libya, Aswan na Luxor nchini Misri, Wadi Halfa nchini Sudan, Mwari Point nchini Namibia na Aoelef nchini Algeria.

Thursday, 5 April 2012

Jakaya Kikwete


Jakaya Mrisho Kikwete alizaliwa Octoba 7 1950 ni mtoto wa sita kwa familia ya watoto 9, ni rais wa 4 na wa sasa wa jamhuri ya Tanzania.Alizaliwa huko Msoga, Bagamoyo Tanganyika ambayo sasa ni Tanzania. Alikuwa pia mwenyekiti wa Umoja wa Afrika toka Januari 31 2008 hadi Februari 2 2009.
Alifuzu na digri ya Uchumi mwaka wa 1975 na kuamua kufanya kazi ya mapato duni kwa chama kilichokuwa kikitawala cha TANU ambapo kikawa ccm, hii ilimpa nafasi kufanya kazi katika maeneo ya vijiji na wilayani.
Kisha slijiunga na Jeshi na kuanza mazoezi katika kambi ya taifa ya Ruvu mwaka 1972. Baada ya kumaliza mazoezi na masomo yake ya kijeshi alikuwa Luteni 1976. Katika kazi yake ya jeshi alipanda ngazi hadi Lieutenat – Colonel. Kuanzia mwaka 1984 hadi 1986, Kikwete alikuwa Mkuu wa Siasa Mwalimu na Commissar wa Siasa katika Chuo cha Kijeshi.
Aliondoka jeshi kama kanali Luteni-wakati vyama vingi vilianza kuingia Tanzania mwaka 1992 na kuamua kuwa mwanasiasa kamili.
Katika siasa za vyama , Kikwete alianza kungaa mwaka 1982 ,wakati alichaguliwa kwa kura nyingi kwa chama cha CCM kuwa mjumbe wa kamati kuu ya taifa sera ya juu na kuwa muamuzi wa chama hicho. Tangu achaguliwe amekuwa akichaguliwa kila baada ya miaka mitano.
Rais Ally Hassan Mwinyi alimteua kuwa mbunge na wakati huo huo, naibu wa Nishati na Madini Novemba 7 1988. Mwaka 1990alipandishwa cheo na kuwa Waziri kamili wa Nishati, Maji na Madini. Baadaye mwaka huo huo, alifanikiwa kugombea kiti cha ubunge katika jimbo la Bagamoyo anapotoka.
1994 akiwa miaka 44 alikuwa waziri wa Fedha nyanga kuwahi kuhudumu katika historia ya Tanzania. Kwenye hazina ya Tanzania aliasisi nidhamu katika usimamizi wa fedha za umma na uwajibikaji hadi leo,yeye hukumbukwa kwa kuanzisha mfumo wa bajeti ya fedha na kufufua miundo ya ukusanyaji wa mapato, mbinu ya taasisi, ikiwa ni pamoja na maandalizi kwa ajili ya malezi.
Desemba 1995, alikuwa Waziri wa Mambo ya Kigeni na ushirikiano wa Kimataifa,akiteuliwa na Rais Benjamin William Mkapa wa serikali awamu ya tatu. Alishikilia wizara hii kwa miaka kumi hadi pale alipote chaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Tanzania Desemba 2005 hivyo kuwa waziri kuwahi kuhudumu katika wizara hiyo kwa muda mrefu katika historia ya Tanzania. Tanzania ilijishugulika kuleta amani katika kanda ya Maziwa Makuu,hususan katika Burundi na Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo. Kikwete pia alikuwa mmoja wa wa wale walioshiriki katika mchakato wa kujenga upya ushirikiano wa kikanda katika Afrika Mashariki.
Utawala wake kama Rais umeshutumiwa kwa kiasi kikubwa cha hongo na kutoshughulikia maswala yanayo wakumba raia wa nchi hiyo.
Ametuhumiwa pia kwa kuchaguwa marafiki wake wa karibu kuwa mawaziri jambo ambalo linamfanya kutowarekebisha wanapoenda kinyume na maadili mema.
Alipokuwa mwenyekiti wa AU changamoto yake kubwa ilikuwa jinsi alivyo shughulikia ghasia zilizo ikumba nchi yetu mwaka 2008.


Amemuowa Mama Salma Kikwete na wana watoto 8.

Vituko


Mama mwenye umri wa miaka 32 amekichoma chumba cha kulala cha bintiye mwenye umri wa miaka 16, akidai kwamba basi la kumpeleka skuli lilikuwa linamwacha. Kulingana na msichana huyo, mamake alibisha mlango kabla ya kutengeneza shimo kwenye mlango na kisha kuwasha moto kwa karatasi na kuingiza kwenye shimo hilo. Moto huo ulichoma kiti chumbani humo.Mama huyo naye aliwaambia askari kwamba mtoto alikuwa anawachwa na basi sasa alifanya hivyo ili msichana wake atoke chumbani humo.

Ukweli Barani


Je wajua, Watu kumi na nane kutoka Afrika wametuzwa na tuzo ya Nobel. Nao wanatoka Algeria, Misri, Ghana, Kenya, Nigeria na Afrika Kusini.

Wednesday, 4 April 2012

Ukweli Barani

Mogadishu, Somalia ni mji wa 4 hatari zaidi dunia. Johannesburg, Afrika Kusini ni  ya 10 hatari zaidi kuishi duniani.

Vituko



Ajuza mmoja wa miaka 70 amemshangaza mtoto wake wa kiume na majirani wake kwa kutongoza kichuna wa kijana wake, na kuvalia mavazi ya kisasa ya kijana na kuongea kwa lugha ya Sheng akisema ''Yo Yo mresh si uko juu manze utamanga nini kuku chipo ama''

Mzee huyo aliyekuwa amevalia Jeans na kusag na tishati kubwa alifaulu kumwingiza kidosho huyo kwenye box

MICHAEL KIJANA WAMALWA

Michael Christopher Wamalwa alizaliwa  eneo la Isiolo, wilayani Bungoma.
Alikuwa mkuu wa wanafunzi na mjadili bora katika shule yake ya sekondari ya Strathmore. Aliibuka kuwa mwanafunzi mwandishi bora nchini na akawakilisha Kenya katika ushindani wa uandishi wa insha huko Uingereza.
Mwaka 1965, alipewa tuzo la masomo ya jamii na kusoma sheria katika Chuo cha Cambridge na kufuzu mwaka 1968.
Alirejea Kenya mwaka 1970 na kuwa mwalimu wa kusomesha elimu ya sheria katika Chuo Kikuu cha Nairobi.
Mwaka wa 1974, alihusika katika kampeini za uchaguzi na kufaulu katika uchaguzi wa 1979. 
Alihusika tena katika kampeini za uchaguzi wa vyama na akachaguliwa kuwa mbunge wa wilaya ya Saboti pamoja na kuwa Makamu wa kwanza wa mwenyekiti wa chama chake.
Baada ya aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha Ford Kenya, Oginga Odinga, kuaga dunia, alifanywa kuwa mwenyekiti wa hicho chama mwaka wa 1994.
Wamalwa alihusika tena katika kampeini za uchaguzi wa 2002 na kufanikiwa kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais, huku Mwai Kibaki akichaguliwa kuwa rais wa Kenya.
Katika mwaka wa 2002, baada ya rais wa Kenya, Mwai Kibaki, kuhusika katika ajali ya barabara na kupelekwa Ulaya ili apate matibabu bora, alimtembelea Mwai Kibaki hospitalini lakini kwa bahati mbaya akaugua figo.
Baada ya kupata nafuu kwa muda mfupi, alifunga pingu za maisha na Yvonne Nambia.
Miezi miwili baada ya harusi yake, akaugua tena na kupelekwa Ulaya katika hospitali ya Royal Free Hospital ambako aliaga dunia masaa ya asubuhi tarehe 23 mwezi Agosti mwaka wa 2003.

Tuesday, 3 April 2012

Vituko



Mwanamke mmoja aliyekuwa akitafutwa sana kwa kumuuwa afisa mmoja amekamatwa kichakani akiwa haja ndogo na kubwa.

Joseph Kabila

Joseph Kabila Kabange alizaliwa kama Hippolyte Kanambe Kazemberembe Kabange Mtwale Juni 4 1971 ni rais wa nne wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Aliingia katika uraisi baada ya kifo cha babake Rais Laurent-Desiree Kabila aliyeuawa na wanajeshi tar. 16 Januari 2001. Wanasiasa wengine walimteua mwana kuwa raisi baada ya baba.



Katika uchaguzi wa kitaifa wa 30 Julai 2006 alipata kura nyingi kuwa raisi lakini hakufikia nusu ya kura zote. Katika uchaguzi wa pili kati yake na Jean-Pierre Bemba alishinda akathebitishwa kuwa rais tar. 17 Novemba 2006. Joseph Kabila ni rais wa kwanza wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo aliyechaguliwa na wananchi wote katika uchaguzi huru.

Joseph Kabila alizaliwa mjini Hewa Bora mkoani wa Kivu Kusini katika mashariki ya Kongo. Babake alikuwa mwanasiasa na kiongozi wa kikundi cha wanamgambo waasi waliopinga serikali ya Mobutu Sese Seko.
Joseph alihamia Dar es Salaam (Tanzania. Alisoma shule ya msingi na ya sekondari katika Dar es salaam na Mbeya na pia alisomea Chuo Kikuu cha Makerere na alisomea Uanajeshi. Octoba 1996 alikuwa Commanda wa kundi la "Kadogos" ambalo ni jeshi la watoto Inasemekana alitumia wakati ule jina la Hippolyte Kanambe Kazemberembe Kabange Mtwale kwa sababu za usalama.


Baada ya ushindi wa wapinzani dhidi ya Mobutu babake alikuwa rais na Joseph alipelekwa masomoni kwenye chuo cha kijeshi huko Uchina. Wakati wa kurudi alipewa cheo cha jenerali jeshini na mwaka 2000 alipandishwa cheo kuwa mkuu wa jeshi.
Alikuwa rais Januari 26 2001 baada ya kifo cha babake Laurent-Desiree Kabila, na kumfanya kuwa rais wa kwanza duniani aliyezaliwa katika miaka ya 1970s. Alikuwa rais mchanga Ulimwenguni hadi januari 2004.
Desemba 2002 alikubali mapatano ya amani kati ya serikali na waasi yaliyokuwa msingi kwa ajili ya kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa na maandalizi ya uchaguzi wa mwaka 2006.
juni 11 2004 mapinduzi ya kijeshi wakiongozwa naye Meja Eric Lenge walijaribu kuchukuwa madaraka na kutangaza kwa radio ya taifa kwamba shughuli zote za serikali zimesitishwa lakini walichindwa na askari wa Kabila.
Desemba 2005 kura ya maoni ya kupitisha katiba mpya ilifanyika na uchaguzi wa rais ulifanyika Julai 30 2006 baada ya kusitishwa kwa tarehe ya hapo awali. Kabila alishinda kwa asilimia 45% naye mpinzani wake na makamu wa rais na mwaasi wa zamani Jean-Pierre Bemba alipata asilimia 20%, Matokeo hayo yalikataliwa na kura zilirudiwa kati ya Kabila na Bemba Oktoba 29.Novemba 15,tume ya uchaguzi ilitangaza matokeo rasmi na Kabila kutangazwa kuwa mshindi na asilimia 58.05% za kura. Matokeo hayo yalithibitishwa na Mahakama Kuu Novemba 27 2006 na kabila kuapishwa Desemba 6 2006 kama rais.
Desemba 2011 Kabila alichaguliwa kwa kipindi cha pili kama rais. Baada ya matokeo kutangazwa tarehe 9 Desemba, kulikuwa na vurugu katika machafuko huko Kinshasa na Mbuji-Mayi ambapo ndiyo iliyo kuwa ngome kuu ya mpinzani wa Kabila Etienne Tshisekedi
Juni Mosi baada ya uvumi mbalimbali kutolewa na maafisa wa nyadhifa za juu serikalini kuhusu ndoa yake,mkuu wa Kaya ya rais, Balozi Theodore Mugalu alitangaza rasmi harusi ya rais na Olive Lembe di Sita.Harusi hiyo ilitendeka Juni 17 2006 wana msichana aliyepewa jina Sifa, jina la mamake Kabila







Uweli barani



Je Wajua Hospitali kubwa zaidi duniani inapatikana Soweto

Monday, 2 April 2012

                       UKWELI KUHUSU AFRIKA
Seychelles ndicho kisiwa ambacho kina idadi ya  watu wachache kabisa duniani(takriban watu 80,000)
                              VITUKO
Mzee mmoja mkaazi wa Texas mwenye umri wa miaka 76 amekamatwa na polisi baada ya kumuua bibi yake pamoja na mbwa wao wawili baada ya mbwa mmoja kati ya hao wawili kujisaidia ndani ya nyumba.
                               MARY ONYANGO
i)Alikuwa makamu mwenyakiti wa tume la shikamano na ushirikiano wa kitaifa.
ii)Alihitimu masomo yke katika Chuo Kikuu cha Nairobi na kupokea shahada ya Biashara. Pia alipokea shahada ya Mambo ya Kifedha kutoka Chuo cha Maastricht nchini Ketherlands
iii)Baada ya kuugua saratani ya matiti, aliungana na marehemu bi. Julia Mulaha ambaye pia laikuwa augua saratani, na kuanzisha programu ya kuwasaidia wanawke wanaougua saratani ya matiti nchini Kenya mwaka 1999.
iv)Akiwa bado katika chuo kikuu, alikuwa muigizaji katika tamthilia mbalimbali kama vile miaha.
                              KWAME NKRUMAH
Kwame Nkrumah alizaliwa mwaka 1909 katika eneo la Nkroful nchini Gold Coast.
Alimaliza masomo yake ya msingi katiika shule ya Achimota iliyoko Accra mwaka 1930, kisha akasomea katika shule ya katoliki ya Roman Catholic Seminary, ambako baadaye alianza kufunza shule moja ya kikatoliki iliyoko Axim.
Katika mwaka 1935, alienda kuendeleza masomo yake katika Chuo Kikuu cha Pennsylvania na kuhitimu masomo yake mwaka 1942.
Kwame alirudi Ghana na kufanywa kuwa katibu mkuu wa chama cha 'United Cold Coast Convention'. Mzozo uliibuka mwaka 1948 tarehe 28 mwezi Februari nchini Chana ambao ulimsababisha kutiwa mbaroni kwani, ilishukiwa kuwa chana cha UGCC ndicho  kilichoanzisha mzozo huo.
Baada ya kuwekwa huru, alifanywa kuwa kiongozi wa Chama cha Vijana mwaka 1948.
Katiba ilirekebishwa  katika mwaka 1952 mwezi Marchi tarehe 10 na Nkrumah akafanywa kuwa waziri mkuu wa kwanza nchini Ghana.
Katika mwaka 1966 mwezi Februari, akiwa bado akizuru nchini Vietnam na China, serikali ya Ghana ikapinduliwa katika mapinduzi ya kijeshi yaliyoanzishwa na Emmanuel Kwasi Kotaka na Baraza la National Liberation Council.
Nkrumah hakurudi Ghana na kuishi uhamishoni nchini Guinea, kama mgeni wa rais wa Guinea, Ahmed Sekou Toure.
Katika mwaka 1972 mwezi Aprili, Nkruma aliugua saratani ya ngozi na kuaga dunia akiwa na umri wa miaka 62.

Tuesday, 27 March 2012

Vituko




Mama wa mtoto mmoja amempa mtoto wake adhabu ya mwaka kwa kumwambia atembee maili mbili akiwa ananyeshewa. Mtoto huyo wa miaka 12 alipewa adhabu hiyo kwa kunywa pombe ya Vodka.

Abdoulaye Wade





Alizaliwa Mai 29 1926 alikuwa rais wa tatu wa Senegali hadi tarehe 25 Marchi 2012 toka mwaka wa 2000.Yeye pia ni katibu mkuu wa chama cha Senegalese party(PDS) na ameongoza chama hicho tangu 1974.Alikuwa kiongozi wa upinzani kwa muda mrefu, na amewania urais mara nne,kuanzia mwaka 1978,kabla ya kuchaguliwa mwaka 2000.Alisomea sheria na kufunza Lycee Condorcet huko Ufaransa.
Wade ana udhamini wa udaktari katika Sheria na uchumi.Alikuwa pia mkuu wa Sheria na Uchumi wa Kitivo katika Chuo Kikuu cha Dakar nchini Senegali.

Amemuowa Viviane Wade. Mwana wao,Karim Wade alikuwa mkuu wa shirika la taifa la Kiislamu,na toka Mei 2009 alihudumu kama Waziri wa Nchi kwa ajili ya Ushirikiano wa Kimataifa,Mijini na Mikoa, Usafiri wa Unga na barabara.Bintiye Sindjely Wade, ni msaidizi maalum wa Rais ambaye alishirikikatika mikutano ya kampeni nyingi kimataifa.

Kufuatia uchaguzi wa 1988, alikamatwa kutokana na maandamano dhidi ya matokeo. Alipokea adhabu ya kusimamishwa kuwania kura.Hatimaye alikwenda Ufaransa, lakini alirudi mwaka 1990.
Aprili 1991, Wade akiwa na jamaa wengine wanne wa chama cha PDS walijiunga na serikali ya umoja wa kitaifa pamoja na chama tawala cha Socialist Party (PS); Wade akawa Waziri wa Nchi bila kupingwa Mnamo Oktoba 1992, yeye na mawaziri wengine wa chama cha PDS wakajiuzulu kwenye serikali kulingana na vile chama tawala cha PS kilivyokuwa kikiongoza serikali.
Uchaguzi wa Februari 1993 Wade alikuwa katika nafasi ya pili na asilimia 32% nyuma ya Diouf ambaye alishinda na asilimia 58%. Octoba mosi , Wade,mkewe na wanachama wa PDS wawili wabunge walikamatwa na kufungwa kutokana na kifo cha makamau wa rais wa baraza la katika. Waliwachiliwa huru baada ya uchunguzi lakini Februari 1994 Wade alikamatwa tena na wanachama wenzake kwa kutishia usalama wa serikali na nchi, waliachiliwa Julai 4 baada ya maandamano ya wafuasi wake.
.
Alijiunga na seikalikama waziri wa Nchi Machi 1995, lakini kama kawa alitoka tena na wafuasi wake wa chama chake cha PDS Machi 1998.Ingawa alichaguliwa kwa Bunge katika uchaguzi Februari 1998 wa bunge, alitangazakujiuzulu kwake kutoka Bunge mwishoni mwa mwezi Julai 1998, akisema kuwa kulikuwa na "manaibu wa kutosha wa kufanya kazi aliyokuwa akifanya.
Katika raundi ya kwanza ya Uchaguzi wa 2000 za urais zilizofanyika Februari 27 alikuwa wa pili tena akipata asilimia 31% za kura lakini kwa mara ya kwanza Diouf hakushinda raundi ya kwanza ya wingi wa kura, na raundi ya pili ikafanyika Machi 19 Wade akashinda na asilimia 58.49% Wade akawa rais Aprili Mosi 2000

Kura za 2007 zilifanywa na pia alishinda, kisha kura za hivi karibuni yaani jumapili mwaka huu zilifanywa lakini alikubali kushindwa.

Ukweli Barani



Nchi kumi masikini Duniani zatoka Afrika.

Monday, 26 March 2012

TABU LEY ROCHEREAU



Alizaliwa mwaka wa 1940, ni mwanamziki kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Yeye ni kiongozi wa Orchestre Afrisa International na kati ya washawishi wakubwa zaidi zaidi katika Sauti na utunzi wa nyimbo pamoja na uandishi wa nyimbo barani Afrika. Pamoja na mchezaji gitaa Dk.Nico Kasanda, walianzisha kundi la Soukous, aliufanya muziki wake ukakubaliwa ulimwenguni kote kwa kucheza muziki wa Kongo na ule wa Cuba, Caribbean na pia Amerika ya Kusini Rumba.

Tabu Ley alizaliwa katika mkoa wa Bandundu, kama Pascal Tabu. Mwaka wa 1954, akiwa na umri wa miaka 18 akiandika wimbo wake wa kwanza Bessama Muchacha ambao alirekodi na Joseph ''Grand Kalle'' kwenye bendi ya Kabasele ya Afrika Jazz. Tabu Ley aliimba wimbo wa Uhuru wa Afrika wa Independence Cha Cha uliotungwa na Grand Kalle wakati Kongo ilipata Uhuru wake mwaka 1960 na kumfanya kuwa maarufu zaidi. Alikaa kwenye bendi hiyo hadi 1963 wakati yeye na Dk. Nico Kasanda waliunda bendi yao Afrikan Fiesta. Miaka miwili baadaye walitawanyika na Tabu Ley kuunda bendi ya Afrikan Fiesta National ambayo ilijulikana pia kama Afrikan Fiesta Flash. Bendi hiyo ikawa yenye mafanikio na bendi iliyojistawi zaidi katika historia ya Afrika kwa kurekodi Afrikan Classic kama Afrika Mokili Mobimba na kupata mauzo zaidi ya nakala millioni moja mwaka 1970. Papa Wemba na Sam Mangwana.
Mwaka wa 1970 Tabu Ley pamoja na Franco walitengeneza bendi ya Orchestre Afrisa International walirekodi nyimbo kama ''Sorozo, ''Kaful Mayay'',''Aon Aon'' na Mose Konzo.

Katika miaka ya 1980 Tabu Ley alikundua talanta mpya ya uimbaji na kucheza, M'bilia Bel ambaye alichangia kuikuza bendi hiyo yake. M'bilia akwa mwanamke wa kwanza barani Afrika kucheza na kuimba Soukous. M'bilia na Tabu Ley walioana na kujaliwa na mtoto mmoja.Mwaka wa 1988 Tabu Ley alileta Mwanamke mwingine wa kuimba anayejulikana kama Faya Tess, kisha mbilia Mbel alijitoa kwenye bendi hiyo na akaendelea kuwa maarufu.Baada ya kutoka M'bilia bendi hiyo na ile ya TPOK Jazz walianza kuwa na upinzani mkubwa zaidi mashabiki nao pia wakagawanya wengi wakikimbilia bendi ilyocheza mtindo mpya wa Soukous.

Mwaka wa 1985, serikali ya Kenya ilipiga marufuku muziki wa kigeni kuchezwa kwenye radio ya taifa, baada ya Tabu Ley kutunga wimbo wa ''Twende Nairobi''(Lets go Nairobi) ulioimbwa naye M'bilia Bel kwa sifa ya rais wa Kenya Daniel Moi, lakini marufuku hayo yalitupiliwa mbali.

Mwaka wa 1990 aliishi Kusini mwa California.akaanza kupeleka muziki wake kimataifa kwa kutunga nyimbo na kuimba kwa Kiingereza na kuoegeza mitindo tofauti kama vile Samba. Alipata maarufu zaidi alipotoa albamu zake kama Muzina, Exil Ley Afrika Worldwide na Babeti Soukous.

Mwaka wa 1996, Tabu Ley alishirikishwa katika albamu Gombo Salsa na kundi la kucheza salsa la Africandos.

Wakati rais Mobutu Sese Seko alipotolewa madarakani mwaka wa 1997 Tabu Ley alirudi Kinshasa na kuwa waziri katika baraza la mawaziri kwa serikali mpya ya rais Laurent Kabila. Kufuatia kifo cha Kabila Tabu Ley alijiunga na bunge maalum la mpito iliyoundwa na Joseph Kabila hadi pale ilipotupilwa mbali.

Novemba 2005 aliteuliwa Makamu Gavana katika maswala ya Kisiasa, Utawala na kijamii na kitamaduni, katika mji wa Kinshasa nafasi iliyopewa chama chake cha Kongo Rally for Democracy kwa mkubaliano wa amani 2002.



Alirudi Ubelgiji kwa kuugua stroke.  

Ukweli Barani Afrika

Mahali ambapo pana joto jingi dunia ni Al'Aziziyah nchini Libya

Vituko



Mwanamke mmoja wa nchi moja ametia fora kwa kuzaa watoto 18 ndani ya miaka 21 ya ndoa yake na mumewe. Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 40 na ushee alijifungua mtoto wake wa 18 jana.

Pamoja na kuwa na watoto 18 mwanamke huyo na mumewe bado hawajaridhika tu na idadi ya watoto walionao na walielezea mpango wao wa kuzaa mtoto wa 19, vyombo vya habari vimeripoti.

Wanandoa hao wana watoto 12 wa kiume na watoto sita wa kike. Mtoto wao wa mwisho ndiye huyo aliyezaliwa jana ikiwa ni wiki moja tu baada ya mtoto wao wa kwanza kusherehekea kutimiza miaka 21.

"Siwezi kusema jinsi ninavyojisikia kuwa na watoto wengi lakini kila mtoto amekuja na baraka zake" alisema mwanamke huyo.

Mwanamke huyo alisema kwamba kwa jinsi alivyoenda kujifungua mara nyingi kwenye hospitali ya Kaplan iliyoko kwenye mji wa Rehovot, manesi wote wa hospitali hiyo wamemzoea sana.

"Tumezoeana sana kiasi cha kwamba utadhani na mimi nafanya kazi hospitali hiyo" alisema mwanamke huyo. 

Friday, 23 March 2012

VITUKO

Mbwa mmoja amewashangaza waumini wa kanisa moja kwa kwenda kanisani na kuketi na kusikiliza neno.Mbwa huyo ambaye alifika mapema na kuketi katika kiti cha kwanza alionekana akifwatilia kila kitu kichokuwa kikitendeka kanisani.

Madilu System


Jean de Dieu Makiese aliyefahamika kama Madilu System , alikuwa muimbaji wa Soukous na muandishi wa nyimbo alizaliwa Léopoldville, Belgian Congo. Alikuwa wakati mmoja katika bendi ya TPOK Jazz,bendi iliyoongoza katika Miziki za Kufana za Afrika kwenye mika za 1960 na 1970.
Alizaliwa Mai 28 1952,na akiwa angali kijana mdogo 1969 Madilu aliimba na kundi la Orchestre Symba, Orchestre Bambula iliyo ongozwa na Papa Noel kisha alitengeneza bendi yake iliyoitwa Orchestre Bakuba Mayopi.
Baadaye alijiunga na Franco na akawa mwanamziki mashuhuri ulimwenguni, Franco ndiye aliyempa jina hilo la Madilu System, jina ambalo lilibaki hadi sasa. Wimbo wake wa kwanza na TPOK Jazz ni ''Mamou(Tu Vois)'' wimbo ambao ulivuma zaidi 1984. kisha ulifwatiwa na wimbo wake mwenyewe ''Pesa Position'' , kisha akatoa wimbo ''Mario'' Mwaka 1985 yeye na Franco walitoa wimbo''Reponse de Mario'' ambao unasemekana ndio wimbo mtamu zaidi kuwahi kuimbwa na wasanii hawa wawili pamoja.
Baada ya kifo cha Franco bendi ya TPOK Jazz aliwacha kurekodi muziki kwa mwaka mmoja. Baadaye bendi hiyo wakaja pamoja chini ya usimamazi wa Madilu System.
Aliaaza kuimba mwenyewe akahamia Pari mji mkuu wa Ufaransa kisha akaenda Geneva Switzerland.
Mwanzoni mwa Agosti 2007, Madilu alisafiri kwenda Kinshasa kupiga video ya nyimbo zake. Alizimia Ijumaa tarehe 10 2007 Agosti. Alipelekwa katika hospitali huko Kinshasa, ambapo aliagaa siku iliyofuatia asubuhi.


UKWELI BARANI



Kuna nchi 54 barani Afrika. Chuo Kikuu cha zamani na cha kale zaidi ulimwenguni kinapatikana mjiini Timbuktu Mali. Katika karne ya 12 Mji huo ulikuwa na vyou vitatu. Zaidi ya wanafunzi 25,000 walisomea kwenye chuo kimoja.

Wednesday, 21 March 2012

VITUKO



Maharusi wamewashangaza jamaa na marafiki baada ya kuwaalika kwenye harusi ya na kupata hawana mavazi ya harusi la wamejichora mwilini kote kama nguo za harusi.

FRANCO LUAMBO LUANZO MAKIADI



Alizaliwa Julai 6 1938 alikuwa jamaa mashuhuru katika karne ya ishirini kwenye muziki wa Kongo, na muziki wa Afrika kwa ujumla. Yeye ni msanii anayejulikana ulimwengu kote kama Franco Luambo ama Franco. Anajulikana sana kwa ustadi wake wa Rumba, alipewa jina la utani 'Mchawi wa Guitar' kwa ajili ya kucheza kwake ala hiyo. Kama muasisi na mwanzilishi wa kundi la OK Jazz anahesabiwa pia kama mwanzilishi wa muziki na sauti ya Kongo.

Alizaliwa katika kijiji cha Sona Bata katika magharibi mwa Bas Zaire ambao sasa ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo siku za ukoloni ikiitwa (Kongo ya Ubelgiji). Alipokuwa bado mtoto wazazi wake walihamia mji mkuu wa Leopoldville (sasa Kinshasa). Babake Joseph Emongo, alikuwa mfanyikazi wa reli wakati mamake alikuwa akipika mikate na kuuza sokoni.Akiwa miaka saba alitengeneza gitaa ambayo alicheza ili kuwavutia wanunuzi katika duka ambalo mamake aliuzia.

Talanta yake ilimsisimua Paul Ebengo Dewayon ambaye alimfunza kucheza ala hiyo. Akiwa miaka 12 alijiunga na kundi la Paul na bendi yake. Miaka mitatu baadaye alitunga rekodi yake ya kwanza Bolingo na ngai na Beatrice (My Love for Beatrice)

Mwaka wa 1955 Franco aliunda bendi yake pamoja na Jean Serge Essous na kuitwa OK Bar huko Leopoldville. Mwaka uliofuatia jina la bendi hiyo likabadilishwa na kuwa OK Jazz kisha likaitwa TPOK Jazz kwa heshima ya mahali lililoazishwa. Basi bendi hiyo ikawa bendi kubwa zaidi kwa muziki wa kongo na likawa na waimbaji 30 kufikia 1980 toka waimbaji 6. Franco alidai kwamba bendi hiyo ilitoa albamu 150 kwa muda wa miak 30 ya bendi hiyo.

Mwaka wa 1958 Franco alitiwa mbaroni, lakini alikuwa ameshakuwa mwimbaji mashuhuri aliachiliwa kutokana na mashabiki wake waliomtaka atolewe jelani.

Franco ameonekana kuwa mfanyabiashara maarufu, na kutengeneza idadi ya makampuni ya kurekodi ya kudhibiti kazi yake mwenyewe na kulea vipaji vipya kama vile (Surboum OK Jazz, Epanza Makita, Boma Bango and Éditions Populaires). Katika miaka ya 1970 muziki wa kikongo ulienea katika Afrika, ukiongozwa na OK Jazz.

Mwaka wa 1980 Franco alitajwa na kupewa jina la ''Grand Master'' wa miziki wa Zaire na Serikali ya nchi hiyo. Jambo hili lilibadilisha mada za nyimbo zake kwa kasi katika kipindi hiki na kuanza kuimba nyimbo za kizalendo na kusifu mashabiki wake matajiri.

Franco alizuru Marekani kwa mara ya kwanza na ya mwisho mwaka wa 1983
Mwaka wa 1985 alitoa wimbo wake mkubwa zaidi Mario, ambao unamaanisha jamaa anayeishi kwa mpenzi wake mzee wa zamani.


Mwaka wa 1987 uvumi ulianza kwamba Franco anaugua sana.Wimbo aliotoa mwaka huo ulikuwa ''Attention Na SIDA''(jihadharini na UKIMWI) kuwaonya kuambukizwa ugonjwa huo,na hivyo kusababisha uvumi lakini bila kudhibitisha kwamba ana virusi vya HIV. Akaanza kutoa nguvu zake kutoka OK Jazz, bendi hiyo ikaanza kurudi chini. Kisha Franco akabadisha dini kutoka kwa Uislamu na kuwa Mkatoliki wa Kirumi. Oktoba 12 1989 aliaga dunia akiwa katika kilinikii ya Ubelgiji. Mwili wake ukasafirisha nyumbani Zaire ambapo jeneza lake lilikuwa limefungwa na bendera ya nchi hiyo polisi walisindikiza mwili wake kwa njia ya barabara na takriban milioni moja wakiomboleza. Serikali ilitangaza siku nne za maombolezo ya kitaifa huku redio zikicheza nyimbo zake tu bila nyimbo zingine. Alizikwa tarehe 17 Oktoba.

Tuesday, 20 March 2012

World Story Telling Day


Leo ni siku ya kusimulia hadithi Ulimwenguni.Katika siku hii watu husimuliana na husikiza hadithi kwa kila Lugha za Ulimwengu.Usiku na Mchana watu huadithiana na hupeana moyo na motisha ili kusoma kitu kuhusu mtu au kitu.

Ni siku ya kipekee Ulimwenguni ambayo watu hujifunza mengi kutokana na hadithi zao, kiini cha siku ya leo ni kuhusu Miti.

Babatunde Olatunji


Alizaliwa Aprili 7, 1927, alikuwa mpiga ngoma, mwanaharakati wa kijamii na msanii wa kurekodi mziki.

Olatunji alizaliwa katika kijiji cha Ajido, mji mdogo karibu na Badagry kusini magharibi mwa Nigeria. Alipata udhamini na kwenda kusomea huko Atlanta mwaka wa 1950.
Ameshinda zawadi nyingi sana katika kazi yake ya muziki.
Alitunga mziki uliotumiwa katika filamu ya Hollywood ya Raisin in the Sun.


Olatunji aliaga dunia mwaka wa 2003 Aprili 6.

VITUKO



Mwanamke mmoja wa miaka 35 ameshtakiwa kwa kuiba chupa mbili za pombe kwenye bar moja. Mwanamke huyo alipatikana akiweka chupa hizo kwenye kwapa zake na chupa ingine alitaka kuweka katikati ya matiti yake.

Monday, 19 March 2012

BAABA MAAL


Alizaliwa Novemba 12 1953 ni mwanamziki kutoka Senegali na mchezaji Guitarist,alizaliwa huko Podor kwenye mto wa Senegali.Licha ya kucheza Guitar yeye pia anawezacheza ala zingine.Ametoa Albamu nyingi sana. Julai mwaka 2003 alifanywa mjumbe wa vijana wa UNDP.

Baaba Maal alitarajiwa kufuata babake na kuwa mvuvi. Hata hivyo, chini ya ushawishi wa maisha yake Mansour Seck rafikiye, Baaba alijitoa mwenyewe kwa kujifunza muziki kutoka kwa mama yake na Mkuu wa shule aliyosomea. Aliendelea kusoma muziki kwenye chuo kikuu katika Dakar kabla ya kuondoka kwa ajili ya masomo ya shahada ya uzamili kwa udhamini katika Beaux-Sanaa mjini Paris.Anajulikana sana barani Afrika na Ulimwenguni kote, huenda akawa mwanamziki maarufu huko Senagali baada ya Youssou N'Dour.

VITUKO



Mama wa mtoto mmoja amempa mtoto wake adhabu ya kusimama kwa barabara na alama zake za mtihani zikiwa zimeandikwa kwenye ubao mkubwa mtoto huyo akiwa ameubeba ili watu waone. Kijana huyo alienda nyumbani na alama mbaya. Babake alimuona mtoto wake akienda barabarani na ubao uliokuwa na maadishi '' Nataka kuwa mtoto mkorofi wa darasa''
Na upande mwingine maadishi yalisoma nipo darasa la nane na nimepata alama ya E kila somo.
Akiwaabia wanahabari wa runinga fulani mtoto huyo alisema nimepata alama ya E kwa darasa langu na kama adhabu napaswa kuwa hapa hadi saa saba.

Thursday, 15 March 2012

UKWELI BARANI





Inajulikana kama reli ndefu ulimwenguni na ni ya Mauritania na ina urefu wa Maili 1.8 yani kilomita 3 na safari hiyo huchukuwa masa 12.

VITUKO




Abiria na wananchi waliozidi elfu 50 wake kwa waume wa nchi fulani hapa Afrika walinunua baskeli kila mmoja na kuendesha baskeli zao wakiwa uchi wa mnyama kisa na maana ni kuwa waendeshaji magari wamekuwa hawajali na ajali za barabara zilizidi. Waendeshaji baskeli hao walijiandika kwenye mwili wao wakisema huu ni mwili wangu.