Pages

Monday, 26 March 2012

TABU LEY ROCHEREAU



Alizaliwa mwaka wa 1940, ni mwanamziki kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Yeye ni kiongozi wa Orchestre Afrisa International na kati ya washawishi wakubwa zaidi zaidi katika Sauti na utunzi wa nyimbo pamoja na uandishi wa nyimbo barani Afrika. Pamoja na mchezaji gitaa Dk.Nico Kasanda, walianzisha kundi la Soukous, aliufanya muziki wake ukakubaliwa ulimwenguni kote kwa kucheza muziki wa Kongo na ule wa Cuba, Caribbean na pia Amerika ya Kusini Rumba.

Tabu Ley alizaliwa katika mkoa wa Bandundu, kama Pascal Tabu. Mwaka wa 1954, akiwa na umri wa miaka 18 akiandika wimbo wake wa kwanza Bessama Muchacha ambao alirekodi na Joseph ''Grand Kalle'' kwenye bendi ya Kabasele ya Afrika Jazz. Tabu Ley aliimba wimbo wa Uhuru wa Afrika wa Independence Cha Cha uliotungwa na Grand Kalle wakati Kongo ilipata Uhuru wake mwaka 1960 na kumfanya kuwa maarufu zaidi. Alikaa kwenye bendi hiyo hadi 1963 wakati yeye na Dk. Nico Kasanda waliunda bendi yao Afrikan Fiesta. Miaka miwili baadaye walitawanyika na Tabu Ley kuunda bendi ya Afrikan Fiesta National ambayo ilijulikana pia kama Afrikan Fiesta Flash. Bendi hiyo ikawa yenye mafanikio na bendi iliyojistawi zaidi katika historia ya Afrika kwa kurekodi Afrikan Classic kama Afrika Mokili Mobimba na kupata mauzo zaidi ya nakala millioni moja mwaka 1970. Papa Wemba na Sam Mangwana.
Mwaka wa 1970 Tabu Ley pamoja na Franco walitengeneza bendi ya Orchestre Afrisa International walirekodi nyimbo kama ''Sorozo, ''Kaful Mayay'',''Aon Aon'' na Mose Konzo.

Katika miaka ya 1980 Tabu Ley alikundua talanta mpya ya uimbaji na kucheza, M'bilia Bel ambaye alichangia kuikuza bendi hiyo yake. M'bilia akwa mwanamke wa kwanza barani Afrika kucheza na kuimba Soukous. M'bilia na Tabu Ley walioana na kujaliwa na mtoto mmoja.Mwaka wa 1988 Tabu Ley alileta Mwanamke mwingine wa kuimba anayejulikana kama Faya Tess, kisha mbilia Mbel alijitoa kwenye bendi hiyo na akaendelea kuwa maarufu.Baada ya kutoka M'bilia bendi hiyo na ile ya TPOK Jazz walianza kuwa na upinzani mkubwa zaidi mashabiki nao pia wakagawanya wengi wakikimbilia bendi ilyocheza mtindo mpya wa Soukous.

Mwaka wa 1985, serikali ya Kenya ilipiga marufuku muziki wa kigeni kuchezwa kwenye radio ya taifa, baada ya Tabu Ley kutunga wimbo wa ''Twende Nairobi''(Lets go Nairobi) ulioimbwa naye M'bilia Bel kwa sifa ya rais wa Kenya Daniel Moi, lakini marufuku hayo yalitupiliwa mbali.

Mwaka wa 1990 aliishi Kusini mwa California.akaanza kupeleka muziki wake kimataifa kwa kutunga nyimbo na kuimba kwa Kiingereza na kuoegeza mitindo tofauti kama vile Samba. Alipata maarufu zaidi alipotoa albamu zake kama Muzina, Exil Ley Afrika Worldwide na Babeti Soukous.

Mwaka wa 1996, Tabu Ley alishirikishwa katika albamu Gombo Salsa na kundi la kucheza salsa la Africandos.

Wakati rais Mobutu Sese Seko alipotolewa madarakani mwaka wa 1997 Tabu Ley alirudi Kinshasa na kuwa waziri katika baraza la mawaziri kwa serikali mpya ya rais Laurent Kabila. Kufuatia kifo cha Kabila Tabu Ley alijiunga na bunge maalum la mpito iliyoundwa na Joseph Kabila hadi pale ilipotupilwa mbali.

Novemba 2005 aliteuliwa Makamu Gavana katika maswala ya Kisiasa, Utawala na kijamii na kitamaduni, katika mji wa Kinshasa nafasi iliyopewa chama chake cha Kongo Rally for Democracy kwa mkubaliano wa amani 2002.



Alirudi Ubelgiji kwa kuugua stroke.  

No comments:

Post a Comment