Pages

Tuesday, 27 March 2012

Abdoulaye Wade





Alizaliwa Mai 29 1926 alikuwa rais wa tatu wa Senegali hadi tarehe 25 Marchi 2012 toka mwaka wa 2000.Yeye pia ni katibu mkuu wa chama cha Senegalese party(PDS) na ameongoza chama hicho tangu 1974.Alikuwa kiongozi wa upinzani kwa muda mrefu, na amewania urais mara nne,kuanzia mwaka 1978,kabla ya kuchaguliwa mwaka 2000.Alisomea sheria na kufunza Lycee Condorcet huko Ufaransa.
Wade ana udhamini wa udaktari katika Sheria na uchumi.Alikuwa pia mkuu wa Sheria na Uchumi wa Kitivo katika Chuo Kikuu cha Dakar nchini Senegali.

Amemuowa Viviane Wade. Mwana wao,Karim Wade alikuwa mkuu wa shirika la taifa la Kiislamu,na toka Mei 2009 alihudumu kama Waziri wa Nchi kwa ajili ya Ushirikiano wa Kimataifa,Mijini na Mikoa, Usafiri wa Unga na barabara.Bintiye Sindjely Wade, ni msaidizi maalum wa Rais ambaye alishirikikatika mikutano ya kampeni nyingi kimataifa.

Kufuatia uchaguzi wa 1988, alikamatwa kutokana na maandamano dhidi ya matokeo. Alipokea adhabu ya kusimamishwa kuwania kura.Hatimaye alikwenda Ufaransa, lakini alirudi mwaka 1990.
Aprili 1991, Wade akiwa na jamaa wengine wanne wa chama cha PDS walijiunga na serikali ya umoja wa kitaifa pamoja na chama tawala cha Socialist Party (PS); Wade akawa Waziri wa Nchi bila kupingwa Mnamo Oktoba 1992, yeye na mawaziri wengine wa chama cha PDS wakajiuzulu kwenye serikali kulingana na vile chama tawala cha PS kilivyokuwa kikiongoza serikali.
Uchaguzi wa Februari 1993 Wade alikuwa katika nafasi ya pili na asilimia 32% nyuma ya Diouf ambaye alishinda na asilimia 58%. Octoba mosi , Wade,mkewe na wanachama wa PDS wawili wabunge walikamatwa na kufungwa kutokana na kifo cha makamau wa rais wa baraza la katika. Waliwachiliwa huru baada ya uchunguzi lakini Februari 1994 Wade alikamatwa tena na wanachama wenzake kwa kutishia usalama wa serikali na nchi, waliachiliwa Julai 4 baada ya maandamano ya wafuasi wake.
.
Alijiunga na seikalikama waziri wa Nchi Machi 1995, lakini kama kawa alitoka tena na wafuasi wake wa chama chake cha PDS Machi 1998.Ingawa alichaguliwa kwa Bunge katika uchaguzi Februari 1998 wa bunge, alitangazakujiuzulu kwake kutoka Bunge mwishoni mwa mwezi Julai 1998, akisema kuwa kulikuwa na "manaibu wa kutosha wa kufanya kazi aliyokuwa akifanya.
Katika raundi ya kwanza ya Uchaguzi wa 2000 za urais zilizofanyika Februari 27 alikuwa wa pili tena akipata asilimia 31% za kura lakini kwa mara ya kwanza Diouf hakushinda raundi ya kwanza ya wingi wa kura, na raundi ya pili ikafanyika Machi 19 Wade akashinda na asilimia 58.49% Wade akawa rais Aprili Mosi 2000

Kura za 2007 zilifanywa na pia alishinda, kisha kura za hivi karibuni yaani jumapili mwaka huu zilifanywa lakini alikubali kushindwa.

No comments:

Post a Comment