
Jean de Dieu Makiese aliyefahamika kama Madilu System , alikuwa muimbaji wa Soukous na muandishi wa nyimbo alizaliwa Léopoldville, Belgian Congo. Alikuwa wakati mmoja katika bendi ya TPOK Jazz,bendi iliyoongoza katika Miziki za Kufana za Afrika kwenye mika za 1960 na 1970.
Alizaliwa Mai 28 1952,na akiwa angali kijana mdogo
1969 Madilu aliimba na kundi la Orchestre Symba, Orchestre Bambula
iliyo ongozwa na Papa Noel kisha alitengeneza bendi yake iliyoitwa
Orchestre Bakuba Mayopi.
Baadaye alijiunga na Franco na akawa mwanamziki
mashuhuri ulimwenguni, Franco ndiye aliyempa jina hilo la Madilu
System, jina ambalo lilibaki hadi sasa. Wimbo wake wa kwanza na TPOK
Jazz ni ''Mamou(Tu Vois)'' wimbo ambao ulivuma zaidi 1984. kisha
ulifwatiwa na wimbo wake mwenyewe ''Pesa Position'' , kisha akatoa
wimbo ''Mario'' Mwaka 1985 yeye na Franco walitoa wimbo''Reponse de
Mario'' ambao unasemekana ndio wimbo mtamu zaidi kuwahi kuimbwa na
wasanii hawa wawili pamoja.
Baada ya kifo cha Franco bendi ya TPOK Jazz aliwacha
kurekodi muziki kwa mwaka mmoja. Baadaye bendi hiyo wakaja pamoja
chini ya usimamazi wa Madilu System.
Aliaaza kuimba mwenyewe akahamia Pari mji mkuu wa
Ufaransa kisha akaenda Geneva Switzerland.

No comments:
Post a Comment