Mama wa mtoto mmoja amempa mtoto wake adhabu ya mwaka kwa kumwambia atembee maili mbili akiwa ananyeshewa. Mtoto huyo wa miaka 12 alipewa adhabu hiyo kwa kunywa pombe ya Vodka.
Tuesday, 27 March 2012
Abdoulaye Wade
Alizaliwa
Mai 29 1926 alikuwa rais wa tatu wa Senegali hadi tarehe 25 Marchi
2012 toka mwaka wa 2000.Yeye pia ni katibu mkuu wa chama cha
Senegalese party(PDS) na ameongoza chama hicho tangu 1974.Alikuwa
kiongozi wa upinzani kwa muda mrefu, na amewania urais mara
nne,kuanzia mwaka 1978,kabla ya kuchaguliwa mwaka 2000.Alisomea
sheria na kufunza Lycee Condorcet huko Ufaransa.
Wade
ana udhamini wa udaktari katika Sheria na uchumi.Alikuwa pia mkuu wa
Sheria na Uchumi wa Kitivo katika Chuo Kikuu cha Dakar nchini
Senegali.
Amemuowa
Viviane Wade. Mwana wao,Karim Wade alikuwa mkuu wa shirika la taifa
la Kiislamu,na toka Mei 2009 alihudumu kama Waziri wa Nchi kwa ajili
ya Ushirikiano wa Kimataifa,Mijini na Mikoa, Usafiri wa Unga na
barabara.Bintiye Sindjely Wade, ni msaidizi maalum wa Rais ambaye
alishirikikatika mikutano ya kampeni nyingi kimataifa.
Kufuatia
uchaguzi wa 1988, alikamatwa kutokana na maandamano dhidi ya matokeo.
Alipokea adhabu ya kusimamishwa kuwania kura.Hatimaye alikwenda
Ufaransa, lakini alirudi mwaka 1990.
Aprili
1991, Wade akiwa na jamaa wengine wanne wa chama cha PDS walijiunga
na serikali
ya umoja wa kitaifa pamoja na chama tawala cha Socialist Party (PS);
Wade akawa Waziri wa Nchi bila kupingwa Mnamo Oktoba 1992, yeye na
mawaziri wengine wa chama cha PDS wakajiuzulu kwenye serikali
kulingana na vile chama tawala cha PS kilivyokuwa kikiongoza
serikali.
Uchaguzi
wa Februari 1993 Wade alikuwa katika nafasi ya pili na asilimia 32%
nyuma ya Diouf ambaye alishinda na asilimia 58%. Octoba mosi ,
Wade,mkewe na wanachama wa PDS wawili wabunge walikamatwa na kufungwa
kutokana na kifo cha makamau wa rais wa baraza la katika.
Waliwachiliwa huru baada ya uchunguzi lakini Februari 1994 Wade
alikamatwa tena na wanachama wenzake kwa kutishia usalama wa serikali
na nchi, waliachiliwa Julai 4 baada ya maandamano ya wafuasi wake.
.
Alijiunga
na seikalikama waziri wa Nchi Machi 1995, lakini kama kawa alitoka
tena na wafuasi wake wa chama chake cha PDS Machi 1998.Ingawa
alichaguliwa kwa Bunge katika uchaguzi Februari 1998 wa bunge,
alitangazakujiuzulu kwake kutoka Bunge mwishoni mwa mwezi Julai 1998,
akisema kuwa kulikuwa na "manaibu wa
kutosha wa kufanya kazi aliyokuwa akifanya.

Kura za 2007 zilifanywa na pia alishinda, kisha kura za hivi karibuni yaani jumapili mwaka huu zilifanywa lakini alikubali kushindwa.
Monday, 26 March 2012
TABU LEY ROCHEREAU
Alizaliwa mwaka wa 1940, ni mwanamziki
kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Yeye ni kiongozi wa
Orchestre Afrisa International na kati ya washawishi wakubwa zaidi
zaidi katika Sauti na utunzi wa nyimbo pamoja na uandishi wa nyimbo
barani Afrika. Pamoja na mchezaji gitaa Dk.Nico Kasanda, walianzisha
kundi la Soukous, aliufanya muziki wake ukakubaliwa ulimwenguni kote
kwa kucheza muziki wa Kongo na ule wa Cuba, Caribbean na pia Amerika
ya Kusini Rumba.

Mwaka wa 1970 Tabu Ley pamoja na Franco
walitengeneza bendi ya Orchestre Afrisa International walirekodi
nyimbo kama ''Sorozo, ''Kaful Mayay'',''Aon Aon'' na Mose Konzo.

Mwaka wa 1985, serikali ya Kenya
ilipiga marufuku muziki wa kigeni kuchezwa kwenye radio ya taifa,
baada ya Tabu Ley kutunga wimbo wa ''Twende Nairobi''(Lets go
Nairobi) ulioimbwa naye M'bilia Bel kwa sifa ya rais wa Kenya Daniel
Moi, lakini marufuku hayo yalitupiliwa mbali.
Mwaka wa 1990 aliishi Kusini mwa
California.akaanza kupeleka muziki wake kimataifa kwa kutunga nyimbo
na kuimba kwa Kiingereza na kuoegeza mitindo tofauti kama vile Samba.
Alipata maarufu zaidi alipotoa albamu zake kama Muzina, Exil Ley
Afrika Worldwide na Babeti Soukous.
Mwaka wa 1996, Tabu Ley alishirikishwa
katika albamu Gombo Salsa na kundi la kucheza salsa la Africandos.
Wakati rais Mobutu Sese Seko
alipotolewa madarakani mwaka wa 1997 Tabu Ley alirudi Kinshasa na
kuwa waziri katika baraza la mawaziri kwa serikali mpya ya rais
Laurent Kabila. Kufuatia kifo cha Kabila Tabu Ley alijiunga na bunge
maalum la mpito iliyoundwa na Joseph Kabila hadi pale ilipotupilwa
mbali.
Novemba 2005 aliteuliwa Makamu Gavana
katika maswala ya Kisiasa, Utawala na kijamii na kitamaduni, katika
mji wa Kinshasa nafasi iliyopewa chama chake cha Kongo Rally for
Democracy kwa mkubaliano wa amani 2002.
Alirudi Ubelgiji kwa kuugua stroke.
Vituko
Mwanamke
mmoja wa nchi moja ametia fora kwa kuzaa watoto 18 ndani ya miaka
21 ya ndoa yake na mumewe. Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 40 na
ushee alijifungua mtoto wake wa 18 jana.
Pamoja na kuwa na watoto 18 mwanamke huyo na mumewe bado hawajaridhika tu na idadi ya watoto walionao na walielezea mpango wao wa kuzaa mtoto wa 19, vyombo vya habari vimeripoti.
Wanandoa hao wana watoto 12 wa kiume na watoto sita wa kike. Mtoto wao wa mwisho ndiye huyo aliyezaliwa jana ikiwa ni wiki moja tu baada ya mtoto wao wa kwanza kusherehekea kutimiza miaka 21.
"Siwezi kusema jinsi ninavyojisikia kuwa na watoto wengi lakini kila mtoto amekuja na baraka zake" alisema mwanamke huyo.
Mwanamke huyo alisema kwamba kwa jinsi alivyoenda kujifungua mara nyingi kwenye hospitali ya Kaplan iliyoko kwenye mji wa Rehovot, manesi wote wa hospitali hiyo wamemzoea sana.
"Tumezoeana sana kiasi cha kwamba utadhani na mimi nafanya kazi hospitali hiyo" alisema mwanamke huyo.
Pamoja na kuwa na watoto 18 mwanamke huyo na mumewe bado hawajaridhika tu na idadi ya watoto walionao na walielezea mpango wao wa kuzaa mtoto wa 19, vyombo vya habari vimeripoti.
Wanandoa hao wana watoto 12 wa kiume na watoto sita wa kike. Mtoto wao wa mwisho ndiye huyo aliyezaliwa jana ikiwa ni wiki moja tu baada ya mtoto wao wa kwanza kusherehekea kutimiza miaka 21.
"Siwezi kusema jinsi ninavyojisikia kuwa na watoto wengi lakini kila mtoto amekuja na baraka zake" alisema mwanamke huyo.
Mwanamke huyo alisema kwamba kwa jinsi alivyoenda kujifungua mara nyingi kwenye hospitali ya Kaplan iliyoko kwenye mji wa Rehovot, manesi wote wa hospitali hiyo wamemzoea sana.
"Tumezoeana sana kiasi cha kwamba utadhani na mimi nafanya kazi hospitali hiyo" alisema mwanamke huyo.
Friday, 23 March 2012
VITUKO
Mbwa mmoja amewashangaza waumini wa kanisa moja kwa kwenda kanisani na kuketi na kusikiliza neno.Mbwa huyo ambaye alifika mapema na kuketi katika kiti cha kwanza alionekana akifwatilia kila kitu kichokuwa kikitendeka kanisani.
Madilu System

Jean de Dieu Makiese aliyefahamika kama Madilu System , alikuwa muimbaji wa Soukous na muandishi wa nyimbo alizaliwa Léopoldville, Belgian Congo. Alikuwa wakati mmoja katika bendi ya TPOK Jazz,bendi iliyoongoza katika Miziki za Kufana za Afrika kwenye mika za 1960 na 1970.
Alizaliwa Mai 28 1952,na akiwa angali kijana mdogo
1969 Madilu aliimba na kundi la Orchestre Symba, Orchestre Bambula
iliyo ongozwa na Papa Noel kisha alitengeneza bendi yake iliyoitwa
Orchestre Bakuba Mayopi.
Baadaye alijiunga na Franco na akawa mwanamziki
mashuhuri ulimwenguni, Franco ndiye aliyempa jina hilo la Madilu
System, jina ambalo lilibaki hadi sasa. Wimbo wake wa kwanza na TPOK
Jazz ni ''Mamou(Tu Vois)'' wimbo ambao ulivuma zaidi 1984. kisha
ulifwatiwa na wimbo wake mwenyewe ''Pesa Position'' , kisha akatoa
wimbo ''Mario'' Mwaka 1985 yeye na Franco walitoa wimbo''Reponse de
Mario'' ambao unasemekana ndio wimbo mtamu zaidi kuwahi kuimbwa na
wasanii hawa wawili pamoja.
Baada ya kifo cha Franco bendi ya TPOK Jazz aliwacha
kurekodi muziki kwa mwaka mmoja. Baadaye bendi hiyo wakaja pamoja
chini ya usimamazi wa Madilu System.
Aliaaza kuimba mwenyewe akahamia Pari mji mkuu wa
Ufaransa kisha akaenda Geneva Switzerland.

UKWELI BARANI
Kuna nchi 54 barani Afrika. Chuo Kikuu cha zamani na
cha kale zaidi ulimwenguni kinapatikana mjiini Timbuktu Mali. Katika
karne ya 12 Mji huo ulikuwa na vyou vitatu. Zaidi ya wanafunzi 25,000
walisomea kwenye chuo kimoja.
Wednesday, 21 March 2012
VITUKO
Maharusi wamewashangaza jamaa na marafiki baada ya kuwaalika kwenye harusi ya na kupata hawana mavazi ya harusi la wamejichora mwilini kote kama nguo za harusi.
FRANCO LUAMBO LUANZO MAKIADI
Alizaliwa Julai 6 1938 alikuwa jamaa mashuhuru katika karne ya ishirini kwenye muziki wa Kongo, na muziki wa Afrika kwa ujumla. Yeye ni msanii anayejulikana ulimwengu kote kama Franco Luambo ama Franco. Anajulikana sana kwa ustadi wake wa Rumba, alipewa jina la utani 'Mchawi wa Guitar' kwa ajili ya kucheza kwake ala hiyo. Kama muasisi na mwanzilishi wa kundi la OK Jazz anahesabiwa pia kama mwanzilishi wa muziki na sauti ya Kongo.
Alizaliwa katika kijiji cha Sona Bata katika magharibi mwa Bas Zaire ambao sasa ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo siku za ukoloni ikiitwa (Kongo ya Ubelgiji). Alipokuwa bado mtoto wazazi wake walihamia mji mkuu wa Leopoldville (sasa Kinshasa). Babake Joseph Emongo, alikuwa mfanyikazi wa reli wakati mamake alikuwa akipika mikate na kuuza sokoni.Akiwa miaka saba alitengeneza gitaa ambayo alicheza ili kuwavutia wanunuzi katika duka ambalo mamake aliuzia.
Talanta yake ilimsisimua Paul Ebengo Dewayon ambaye alimfunza kucheza ala hiyo. Akiwa miaka 12 alijiunga na kundi la Paul na bendi yake. Miaka mitatu baadaye alitunga rekodi yake ya kwanza Bolingo na ngai na Beatrice (My Love for Beatrice)
Mwaka wa 1955 Franco aliunda bendi yake pamoja na Jean Serge Essous na kuitwa OK Bar huko Leopoldville. Mwaka uliofuatia jina la bendi hiyo likabadilishwa na kuwa OK Jazz kisha likaitwa TPOK Jazz kwa heshima ya mahali lililoazishwa. Basi bendi hiyo ikawa bendi kubwa zaidi kwa muziki wa kongo na likawa na waimbaji 30 kufikia 1980 toka waimbaji 6. Franco alidai kwamba bendi hiyo ilitoa albamu 150 kwa muda wa miak 30 ya bendi hiyo.
Mwaka wa 1958 Franco alitiwa mbaroni, lakini alikuwa ameshakuwa mwimbaji mashuhuri aliachiliwa kutokana na mashabiki wake waliomtaka atolewe jelani.
Franco ameonekana kuwa mfanyabiashara maarufu, na kutengeneza idadi ya makampuni ya kurekodi ya kudhibiti kazi yake mwenyewe na kulea vipaji vipya kama vile (Surboum OK Jazz, Epanza Makita, Boma Bango and Éditions Populaires). Katika miaka ya 1970 muziki wa kikongo ulienea katika Afrika, ukiongozwa na OK Jazz.
Mwaka wa 1980 Franco alitajwa na kupewa jina la ''Grand Master'' wa miziki wa Zaire na Serikali ya nchi hiyo. Jambo hili lilibadilisha mada za nyimbo zake kwa kasi katika kipindi hiki na kuanza kuimba nyimbo za kizalendo na kusifu mashabiki wake matajiri.
Franco alizuru Marekani kwa mara ya kwanza na ya mwisho mwaka wa 1983
Mwaka wa 1985 alitoa wimbo wake mkubwa zaidi Mario, ambao unamaanisha jamaa anayeishi kwa mpenzi wake mzee wa zamani.

Tuesday, 20 March 2012
World Story Telling Day
Leo ni siku ya kusimulia hadithi Ulimwenguni.Katika siku hii watu husimuliana na husikiza hadithi kwa kila Lugha za Ulimwengu.Usiku na Mchana watu huadithiana na hupeana moyo na motisha ili kusoma kitu kuhusu mtu au kitu.
Ni siku ya kipekee Ulimwenguni ambayo watu hujifunza mengi kutokana na hadithi zao, kiini cha siku ya leo ni kuhusu Miti.
Babatunde Olatunji
Alizaliwa Aprili 7, 1927, alikuwa mpiga ngoma, mwanaharakati wa kijamii na msanii wa kurekodi mziki.
Olatunji alizaliwa katika kijiji cha Ajido, mji mdogo karibu na Badagry kusini magharibi mwa Nigeria. Alipata udhamini na kwenda kusomea huko Atlanta mwaka wa 1950.
Ameshinda zawadi nyingi sana katika kazi yake ya muziki.
Alitunga mziki uliotumiwa katika filamu ya Hollywood ya Raisin in the Sun.
VITUKO
Mwanamke mmoja wa miaka 35 ameshtakiwa kwa kuiba chupa mbili za pombe kwenye bar moja. Mwanamke huyo alipatikana akiweka chupa hizo kwenye kwapa zake na chupa ingine alitaka kuweka katikati ya matiti yake.
Monday, 19 March 2012
BAABA MAAL

Baaba
Maal alitarajiwa kufuata babake na kuwa mvuvi. Hata hivyo, chini ya
ushawishi wa maisha yake Mansour Seck rafikiye, Baaba alijitoa
mwenyewe kwa kujifunza muziki kutoka kwa mama yake na Mkuu wa shule
aliyosomea. Aliendelea kusoma muziki kwenye chuo kikuu katika Dakar
kabla ya kuondoka kwa ajili ya masomo ya shahada ya uzamili kwa
udhamini katika Beaux-Sanaa mjini Paris.Anajulikana sana barani
Afrika na Ulimwenguni kote, huenda akawa mwanamziki maarufu huko
Senagali baada ya Youssou N'Dour.
VITUKO
Mama wa mtoto mmoja amempa
mtoto wake adhabu ya kusimama kwa barabara na alama zake za mtihani
zikiwa zimeandikwa kwenye ubao mkubwa mtoto huyo akiwa ameubeba ili
watu waone. Kijana huyo alienda nyumbani na alama mbaya. Babake
alimuona mtoto wake akienda barabarani na ubao uliokuwa na maadishi
'' Nataka kuwa mtoto mkorofi wa darasa''
Na upande mwingine maadishi
yalisoma nipo darasa la nane na nimepata alama ya E kila somo.
Akiwaabia wanahabari wa
runinga fulani mtoto huyo alisema nimepata alama ya E kwa darasa
langu na kama adhabu napaswa kuwa hapa hadi saa saba.
Thursday, 15 March 2012
UKWELI BARANI
Inajulikana
kama reli ndefu ulimwenguni na ni ya Mauritania na ina urefu wa Maili
1.8 yani kilomita 3 na safari hiyo huchukuwa masa 12.
VITUKO
Abiria na wananchi waliozidi elfu 50 wake kwa waume wa nchi fulani hapa Afrika walinunua baskeli kila mmoja na kuendesha baskeli zao wakiwa uchi wa mnyama kisa na maana ni kuwa waendeshaji magari wamekuwa hawajali na ajali za barabara zilizidi. Waendeshaji baskeli hao walijiandika kwenye mwili wao wakisema huu ni mwili wangu.
GRACE OGOT
Ni
mwandishi, Nesi, Mwandishi wa habari, Mwanasiasa na Mwanadiplomasia
kutoka Kenya.

Tangu
wakati huo ameshikilia nyadhifa mbalimbali za ubalozi kwani
amewakilisha nchi yake katika Umoja wa Mataifa na UNESCO. Alikuwa
mwanachama mwanzilishi wa shirika la Waandishi wa Kenya maarufu kwa
Kiingereza kama Writers' Association of Kenya.
Grace
Ogot aliyezaliwa 1934 alifunga ndoa na mwanahistoria Profesa Bethwell
Allan Ogot, kutoka sehemu ya Gem, mnamo mwaka wa 1959 na ni mama wa
watoto wanne.
Kitabu
chake cha kwanza kilikuwa Land Without Thunder kitabu cha hadithi
fupi. Riwaya yake ya kwanza ilikuwa The Promised Land.
Wednesday, 14 March 2012
Charity Ngilu
Charity Ngilu Kaluki alizaliwa 1952, ni
mwanasiasa kutoka Kenya. Alikuwa waziri wa Afya kutoka 2003 hadi 2007
na aliteuliwa waziri wa Maji Aprili 2008.
Alizaliwa kule mbooni wilayani Makueni
1952, alipata elimu yake kwenye shule ya upili ya Alliance High
School, kisha alifanya kazi kama karani wa wa benki ya Central ya
Kenya kabla ya kuanzisha biashara yake.
Katika uchaguzi wa kwanza wa vyama
vingi hapa nchini mwaka1992 aliwashangaza wengi kwa kupita kura za
Kitui ya kati katika chama cha Democratic Paty.

Baadaye alijiunga na chama cha National
Party of Kenya. Uchaguzi wa 2002 chama chake kilikuwa miongoni mwa
vyama vilivyo tengeneza NARC muungano huo wa NARC ulishinda uchaguzi
huo na Mwai Kibaki alimteuwa waziri wa Afya Januari 3 2003.
Julai 31 2007 Ngilu alimpeleka Ann
Njogu mwandamaji hospitalini baada ya kupigwa na polisi, kisha
alihutumiwa na kukashifiwa kwa madai ya kumtorosha Njogu polisini,
alikamatwa na kufungwa Agosti 12 na kisha kutoka kwa thamani.
Oktoba 5,2007 ngilu alitangaza kujiunga
na ODM na mwaniaji urais wa chama hicho Raila Odinga katika kura za
2007 na alimlinganisha Bw Odinga na Bw Nelson Mandela.
Bwanake Micheal Mwendwa Ngilu aliaga
Julai mosi, 2006 Afrika Kusini na ana watoto watatu.
VITUKO
Mtoto wa miaka 8
amewashangaza waziziwe na majirani kwa kuvuta sigara. Babake msichana
huyo anasema aliaza kuvuta sigara akiwa na umri wa miaka 4, na sasa
yeye huvuta hadi packeti 2 kila siku na asipovuta sigara huanza
kulia.
UKWELI BARANI.
Wanyama wanne wa
porini ambao wana mbio zaidi wanapatikana barini afrika, Miongoni ni
Duma, Simba,WildBeest, na Thomson's gazelle. Wanyama hawa wote wana
mbio zaidi ya maili 50 kwa lisali moja, na Duma akiweza kufikisha
maili 70 kwa lisali.
Tuesday, 13 March 2012
Martha Karua.
Martha Wangari Karua alizaliwa 22 Septemba 1957, ni mwanasiasa kutoka Kenya na pia ni mbunge wa Gichugu na wakili wa mahakama kuu ya Kenya. Alikuwa waziri wa Sheria lakini alijiuzuli mnamo Aprili 2009.

Alifanya kazi
katika mahakama ya hakimu wilayani na kupanda ngazi hadi Hakimu mkazi
Mwandamizi hadi alipotoka 1987. Katika kipindi hiki, alikuwa alikuwa
msimamizi wa mahakama za sheria Makadara 1984 – 1985 na Mahakama za
Kibera 1986 – 1987.
Yeye alichangia
kwa kiasi kikubwa maendeleo ya sheria ya familia na hasa ugawaji wa
mali ya ndoa pamoja na sheria ya kikatiba na utawala.
Kutoka mwaka wa
1990 – 2002 alikuwa mwanachama wa harakati za upinzani wa kisiasa
ambao walipigania demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya katika miaka
ya 1990 wakati Kenya ilikuwa chini ya utawala wa Daniel Moi.
Alikuwa mmoja
wa waliotengeneza chama cha NARC kilichoshinda kura za 2003 na
kumaliza miongo minee ya utawala wa KANU.
Alichaguliwa
kuwa mwenyekiti wa NARC Novemba 15 2008.
Alikuwa waziri
wa kwanza kujiuzulu kwa hiyari yake tangu 2003.
UKWELI BARANI
Karibia asilimia 90 za kasi za Malaria
duniani kote hutokea Afrika, na watoto 3,000 kutoka Afrika hufariki
kila siku kutokana na mathara yake.
VITUKO
Mwanamme mmoja alijipangia kifo chake
alipopigwa na risasi karibu na kaburi lake alilojichimbia. Imebaki
haijulikani kama alipanga ama ilikuwa kwa bahati mbaya.
Friday, 9 March 2012
TIRUNESH DIBABA
![]() |
Dibaba |
Pia
anajulikana kama Tirunesh Dibaba Kenene alizaliwa Oktoba 1 1985 huko
Bekoji, Arsi Uhabeshini (Ethiopia). Ni mwanariadha wa masafa marefu.
Kwa sasa Ndiye bingwa wa Olompiki kwa mbio za mita 5000 na mita
10,000, amepewa jina la utani 'Baby Faced Destroyer'.
Alizaliwa
katika kijiji cha Bekoji, Dibaba ni mtoto wa 4 kwa watoto 6. Alianza
riadha akiwa na umri wa miaka 14, na alihamia mji mkuu wa Addis Ababa
mwaka 2000.
Dibaba
anatoka kwa familia ya wanariadha dada zake na ndugu zake pia wakiwa
kwenye nyanja hiyo ya riadha.
Dibaba
amepata mafanikio makubwa katika michuano ya dunia matukio ya riadha
ya 2003,2006 na 2007.
Aliweka
upya rekodi ya dunia katika mbio za mita 5000 kwa muda wa 14:11.15
katika mkutano wa Oslo Golden League mwaka 2008.

Wiki
moja baadaye akashinda mbio za mita 5000 Agosti 22 2008.
Dibaba
ameolewa kwa mshindi wa mbio za Olimpiki wa mwaka wa 2004 na 2008
Sileshi Sihine.
VITUKO
Polisi huyo aliyeaga ameshtakiwa kwa kukubali rushwa ya shillingi elfu 100,000 kutoka kwa binamu wa jambazi sugu wa mtaa huo ambaye alikuwa anasakwa sana..
Aliaga kwa mshtuko wa moyo miaka miwili kabla ya kesi hiyo.
Jaji wa kesi hiyo aliambia koti kwamba watu waliofariki hawawezi toa ushuhuda.lakini atiwe pingu akiwa kwenye kaburi lake.
UKWELI BARANI
Zaidi
ya watu milioni 17 katika Afrika kusini mwa Sahara wamefariki
kutokana na UKIMWI, na wataalamu wanakadiria kuwa angalau zaidi ya
watu milioni 25 wana UKIMWI kutoka Afrika.
Thursday, 8 March 2012
BENJAMIN MKAPA
Mkapa alizaliwa mwaka wa 1938 huko Ndanda Tnzania kusini. Alihitimu kutoka Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda mwaka 1962 na shahada ya Kiingereza. Pia alihudhuria Chuo Kikuu cha Columbia mwaka 1963 na akatuzwa shahada yake katika masuala ya kimataifa.
Alikuwa ni afisa wa utawala wa Dodoma na waziri wa Teknolojia ya Sayansi na Elimu ya juu.
Tangu mwaka 1977 hadi 1990 alikuwa ni Waziri wa mambo ya kigeni.
Katika mwaka wa 1995, Mkapa alichaguliwa kuwa rais wa Tamzania kwa kufuatilia misingi ya kampeni maarufu ya kupambana na rushwa na kuwa mfuasi mwamini wa aliyekuwa rais wa Tanzania Julius Nyerere.
Mkapa alitoa juhudi za kupambana na rushwa na kuumba jukwaa la wazi la Rushwa la Tume ya Rais.
Akiwa bado rais, Mkapa alibinafsisha mashirika ya serikali na akaweka sera za soko huru,
Wafuasi wake walisema kuwa kuvutia uwekezaji wa kigeni ungesaidia kukuza uchumi.
Sera zake zilipata msaada wa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani na kusababisha kufutwa kwa baadhi ya madeni ya kigeni ya Tanzania.
Uongozi wake kama rais wa Tanzania ulifika kikomo mwezi Desemba mwaka 2005.
VITUKO
Huku wanawake wakisherehekea siku
yao Duniani mwanamke mmoja Nchini Zimbabwe amewashangaza watu kwa
kutaka kufunga ndoa na kumuowa mwanawe mwenye umri wa miaka 24.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka
42 alisema kwamba wakati bwanake aliaga miaka 6 iliyopita hakuna mtu
yeyote alimsaidia kumsomesha mwanawe na sasa hataki msichana yeyote
kumkaribia mwanawe eti kwa sababu ana kazi. Kuongeza maji kwenye Unga
mwanamke huyo amesema tayari ni mja mzito na miezi sita na mwanawe.
Mwanamke huyo alisema ndugu za
marehemu bwanake walionyesha hari ya kumrithi lakini yeye hataki
anataka mwanawe, basi mwanawe pia amekubali atamuowa mamake.
SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Nchi zingine kama Uchina, Russia,
Vietnam na Bulgaria siku ya leo ni sikuku ya kitaifa.
Siku hii wanawake wanaadhimisha miaka
101 tangu siku hii izinduliwe.
Kiini cha siku hii ni 'Connecting
Girls, Inspiring Future' Yaani KUUNGANISHA WASICHANA KUHIMIZA HATIMA
BAADHI
TU YA WANAWAKE WALIOFUZU KWA NYANJA MBALIMBALI
Luisa
Diogo ni Waziri Mkuu wa nchi ya Mozambique .
Ellen
Sirleaf-Johnson ndiye rais wa kwanza mwanamke barani Afrika wa nchi
ya Liberia.
Sylvie
Kinigi ndiye mwanamke wa kwanza kuwa Waziri Mkuu barani Afrika wa
nchi ya Burund.
Wanawake
wanashikilia asilimia 18% za nyadhifa za ubunge Ulimwenguni,
Marekani
ipo katika nafasi ya 68 kwa mataifa 134 ulimwenguni kwa asilimia
16.8% ya wanawake ambao wapo bungeni.
Oktoba
2003 nchi ya Rwanda ndio nchi iliyo karibia idadi ya wanawake kwa
wanaume bungeni.
Kwa
Serikali 189 Duniani kuna wanawake 13 ambao wanashikilia nyadhifa za
juu sana.ambao ni
- Angela Merkel, Chancellor of Germany
- Cristina Fernández de Kirchner, President of Argentina
- Ellen Johnson-Sirleaf, President of Liberia
- Gloria Macapagal-Arroyo, President of the Philippines
Helen Clark, Prime Minister of New Zealand
- Luisa Diogo, Prime Minister of Mozambique
- Mary McAleese, President of Ireland
- Micheline Calmy-Rey, President of the Swiss Confederation
- Michelle Bachelet, President of Chile
- Pratibha Patil, President of India
- Tarja Halonen, President of Finland
- Yulia Tymoshenko, Prime Minister of Ukraine
- Zinaida Greceanîi, Prime Minister of MoldovaFACTS ABOUT WOMENKwa watu milioni 876 ya waliosoma kwa nchi zilizostawi duniani thulithi mbili ni wanawake.Wanawake hukuza ama huzalisha nusu ya chakula duniani lakini wana asilimia moja tu ya shamba.Katika nchi ya Saudi Arabia mwanake anaweza kupa talaka mme wake iwapo hatampa chai.
Mwanamke aliye stawi ana viatu 20, ambavyo viatu 11 kwa hivyo hatawahi vivaa.
Wanawake huongea mara tatu zaidi ya wanaume, Uchunguzi umeonchesha kwamba wanawake takriban maneno 20,000 kwa siku, na wanaume maneno 7,000
Wanawake huchukua takriban miaka 2 ya maisha yao wakijiangalia kwenye kioo, na wao husema kwamba Tv sio nzuri kama ilivyokuwa hapo zamani
HISTORYSiku ya Wanawake Duniani ni siku ya kimataifa inayosherehekea mafanikio ya kiuchumi, kisiasa na kijamii ya wanawake kutoka vizazi vilivyopita, vya sasa na vya baadaye.
Mashirika, serikali na mashirika ya wanawake kote duniani huchagua mandhari tofauti kila mwaka kwa kutafakari masuala ya jinsia ya kimataifa na serikali za mitaa.
Siku hii ilianza kusherehekewa katika miaka ya 1910.
Siku hii ya wanawake ilisherehekewa Machi 19 ,1911 huko Ujerumani, Australia, Denmark na nchi zingine za ulaya. Wanawake wa nchi zii walisherehekea siku hii kwa sababu ya wanawake kunyimwa haki za kupiga kura na mfalame wa nchi ya Prussian.
Kiini cha kutenga siku hii ilikuwa nikuwapa uhuru wa kupiga kuaUhuru wa kutoa maoni yaoUhuru wa kufanya kazi kwa ofisi za umaUhuru wa kwenda shule miongoni maswala mengi.Tunaposherehekea siku 101 ya wanawake Shirika la wanawake la Kenya FIDA wamesema wanachukuwa fursa hii kuangalia mafanikio wanawake wamepata.

TEKLA LORUPE CHEPKITE
Alizaliwa Mei 9 1973 katika Kutomwony
Kenya, ni mkimbiaji wa mbio za masafa marefu na msemaji wa kimataifa
kwa ajili ya amani, haki za wanawake na elimu.
Lorupe anashikilia rekodi ya dunia kwa
kilomita 20,25 na 30 na hapo awali alishikilia rekodi ya marathon
duniani. Ni bingwa wa wa marathon duniani na alikuwa mwanamke
mwafrika wa kwanza kushinda mbio za marathon za New York ambazo
ameshinda mara mbili.Ameshinda marathon katika miji kama London,
Boston, Hong Kong, Berlin, Rome na nchi nyingine nyingi.
Utotoni mwake alikuwa akienda shambani,
akichunga ngombe na kuwaangalia baadhi ya ndugu na dada zake. Ana
Ndugu na Dada 24, alianza shule akiwa na umri wa miaka 6 na alikuwa
akikimbia kilomita 10 kwenda na kurudi shuleni. Alijua ana kipaji cha
ukimbiaji akiwa shuleni akishiriki katika mbio za mita 800 na 1500 na
wanafunzi amboa wengine walikuwa wakimshinda kwa umri.
Kutokana na hayo alianza ukimbiaji
lakini bila usaidizi wa mtu yeyote, Mwaka 1994 na 1998 alishinda mbio
za Goodwill zaidi ya mita 10,00 bila viatu. Kwa umbali huo huo
alishinda medali ya shaba katika mashindano ya Dunia ya IAAF mwaka
1995 na 1998.
Mwaka wa 2006 alitajwa na katibu wa
umoja wa mataifa wakati ule Koffi Annan kama balozi wa michezo wa
umoja wa mataifa pamoja na Roger Federer bingwa wa Tennis kutoka
Uswisi.
UKWELI KUHUSU WANAWAKE
Mwanamke huhitaji kulia na hawezi kufanya hivyo kama hakuna wa kumsikia na kumtuliza.
Mwnawamke hutishika sana na swala la uzito wake kimwili.Kila wakati lazima ajiangalie ameongeza au amepunguza.
Mwanamke hupenda kutengeneza nywele zake vilivyo kabla kulala.
Wanawake hupenda kupiga ngumzo ingawaje wanachozungumzia kinaweza kuwa hakina maana yeyote.
Wanawake daima huuliza maswali yasiyokuwa na majibu sahihi kwa jitihada za kumfanya mtu kupata hisia za hatia moyoni mwake.
Mwanamke ni mtu ambaye anapenda kufanya shopping ama vitu ukipenda hususan rejareja.
Mwanamke ni mtu anaye chukia mende (KOMBAMWIKO) .
Mwanamke ni mtu asiyeweza kukosa kujibu simu.
Mwnawamke hutishika sana na swala la uzito wake kimwili.Kila wakati lazima ajiangalie ameongeza au amepunguza.
Mwanamke hupenda kutengeneza nywele zake vilivyo kabla kulala.
Wanawake hupenda kupiga ngumzo ingawaje wanachozungumzia kinaweza kuwa hakina maana yeyote.
Wanawake daima huuliza maswali yasiyokuwa na majibu sahihi kwa jitihada za kumfanya mtu kupata hisia za hatia moyoni mwake.
Mwanamke ni mtu ambaye anapenda kufanya shopping ama vitu ukipenda hususan rejareja.
Mwanamke ni mtu anaye chukia mende (KOMBAMWIKO) .
Mwanamke ni mtu asiyeweza kukosa kujibu simu.
Wednesday, 7 March 2012
UKWELI BARANI
Ishara
ama alama za samaki hutumika kama njia za kuwafukuza pepo ama
mashetani huko Tunisia. Majumba mapya yana mifupa ya samaki ama mkia
wa samaki yanapojengwa, na magari pia yana michoro ya samaki ili
kuwapa usalama wanaosafiri.
David Rudisha
David
Lekuta Rudisha alizaliwa Decemba 17 1988 ni mkimbiaji wa Kenya na ana
rekodi ya dunia katika mbio za mita 800 kwa muda wa 1:41.01. Rudisha
pia anashikilia rekodi nne za mbio kumi bora ulimwenguni.
Kazaliwa
katika Kovai Wilaya ya Transs Mara, alipata elimu yake katika shule
ya upili ya Mtakatifu Francis Kimuron huko Iten Wilaya ya Keiyo,
ambayo pia imekuza na kuwalea wakimbiaji kadhaa. Awali alikuwa
mkimbiaji wa mita 400 lakini kocha wake alimsababisha kujaribu mita
800.
Mwaka
wa 2006 akawa bingwa wa dunia katika kitengo cha junior cha umbali
huo.

Rudisha
sasa anashikilia rekodi ya dunia kwenye mbio mita 800 alivunja rekodi
ya hapo awali iliyokuwa imewekwa mwka wa 2007 kwenye mbio za ISTAF
IAAF World Challenge huko Berlin Agosti 22 2010 kwa muda wa 1:41.09.
Rekodi ya hapo awali ikishikiliwa na mzaliwa wa Kenya lakini hivi
sasa ni raiya wa Denmark Wilson Kipketer. Rudisha alivunja rekodi
hiyo kwa sekunde 0.02.
Novemba
2010 akiwa na umri wa miaka 21 alikuwa mkimbiaji mchanga duniani
kuwahi kushinda tuzo la mkimbiaji bora Duniani la IAAF, alishinda
pia mwanaspoti bora wa mwaka Kenya.
Rudisha
ni mwanachama wa kabila la wamaasai, babake Daniel Rudisha mkimbiaji
mstaafu aliyeshinda nishani ya fedha katika mbio za Olympiki mwaka
1968 katika mbio za rely za 4 x400 wakati mamake ni mstaafu wa mbio
za mita 400.
Amemuowa
Lizzy Naanyu na wana binti mmoja.
KIZZA BESIGYE

Alihitimu masomo yake na kupata shahada ya udaktari karika mwaka wa 1980.
Baada ya kuwacha kazi kaika hospitali ya Aga Khan iliyoko Nairobi nchini kenya, alifanya mazoezi ya kigeshi mwaka wa 1980-1986 na kujiunga na kundi la jeshi la National Resistance Army.
Katika mwaka wa 1986, alichaguliwa kuwa waziri wa Mambo ya Ndani na aliyekuwa rais wa Uganda kwa wakati huo,ambaye bado ni rais wa Uganda kwa wakati huu, Yoweri Museveni. Kisha akachaguliwa kuwa waziri wa Nchi katika ofisi ya rais.
Katika mwaka wa 1991, akawa afisa mkuu wa kikosi cha kisasa katika Masaka na katika mwaka wa 1993, akawa Mkuu wa Vifaa na Uhandisi.
Katika mwaka wa 1998, Besigye alimwoa Winnie Byanyima, ambaye alikuwa mbunge wa Manispaa ya Mbarara na mwanamke mhandisi wa kwanza nchini Uganda, na wakajaliwa na mtoto wa kiume kwa jina Anselm Besigye.
Katika uchaguzi wa rais mwaka wa 2001, Besigye alikuwa miongoni mwa waliowania kiti cha urais na kwa bahati mbaya, hakufaulu katika huo uchaguzi na Museveni akaibuka kuwa mshindi na akachaguliwa kuwa rais wa Uganda.
Katika tarehe 23 mwezi Marchi mwaka 2001, Besigye alipinga matokeo ya huo uchaguzi katika Mahakama Kuu ya Uganda, akitoa mfano wa wizi mkubwa na ghasia za uchaguzi na Museveni lakini hakufaulu.
Besigye alikamatwa na kutiwa mbaloni na askari katika tarehe 30 mwezi Juni mwaka 2001, kwa kuhutumiwa kuwa na kosa la uhaini.
Alikimbilia ulaya katika mwezi wa Septemba ili kuokoa maisha yake yaliyokuwa hatarini.
Katika mwaka wa 2005 tarehe 26 mwezi Oktomba, Besigye alirudi nyumbani kutoka Afrika Kusini alikokuwa akiishi.
Katika uchaguzi mkuu uliofanyka mwaka wa 2006, Besigye kwa mara ya pili aliwania kiti cha rais na kutofanikiwa. Museveni alipata kura za asilimia 59 ilhali Besigye alipata kura za asilimia 37.
Besigye alipoteza kura kwa mara ya tatu katika uchaguzi wa 2011 ambao Yoweri Museveni bado aliibuka kuwa mshindi.
Katika tarehe 28 mwezi Aprili, Besigye alikamatwa na polisi baada ya kuanzisha maandamano dhidi ya bei ghali za chakula na mafuta.
Tuesday, 6 March 2012
MICHAEL DEMITRI SHALHOUB

Mwigizaji katika sinema ya Lawrence of Arabia mwaka 1962,alizaliwa tarehe 10 mwezi Afril mwaka 1932 huko Alexandria nchini Misri.
Alipata elimu yake katika chuo cha Victoria huko Alexandria na kisha kusomea shahada ya hisabati na fizikia katika chuo kikuu cha Cairo.
Baada ya kuhitimu masomo yake, alijiunga na biashara ya familia.
Kabla ya kutoa filamu debut kwa lugha ya kiingereza, tayari alikuwa amenawiri nchini Misri na pia kimataifa.
Mwaka 1953, alikutana na muigizaji wa kike maarufu nchini Misri, Faten Hamama na hilo lilimlazimu kubadili dini na hapo ndipo alipojipatia jina Omar-al-Sharif.
Je wajua hata baada ya Sharif kubadili dini ili amuoe Faten Hamama walijaaliwa na mtoto mmoja na kutalakiana 1974.
Mwaka 2003 Augosti, alifungwa mwezi mmoja jela kwa kosa la kumpiga afisa wa polisi katika kilabu cha casino-Subburbar Paris mwezi Julai. Na kama haitoshi aliamuriwa kulipa faini ya shillingi 141,697.70 pesa za Kenya na kumlipa polisi elfu 28,339.54-pesa za Kenya.
Subscribe to:
Posts (Atom)