Charity Ngilu Kaluki alizaliwa 1952, ni
mwanasiasa kutoka Kenya. Alikuwa waziri wa Afya kutoka 2003 hadi 2007
na aliteuliwa waziri wa Maji Aprili 2008.
Alizaliwa kule mbooni wilayani Makueni
1952, alipata elimu yake kwenye shule ya upili ya Alliance High
School, kisha alifanya kazi kama karani wa wa benki ya Central ya
Kenya kabla ya kuanzisha biashara yake.
Katika uchaguzi wa kwanza wa vyama
vingi hapa nchini mwaka1992 aliwashangaza wengi kwa kupita kura za
Kitui ya kati katika chama cha Democratic Paty.

Baadaye alijiunga na chama cha National
Party of Kenya. Uchaguzi wa 2002 chama chake kilikuwa miongoni mwa
vyama vilivyo tengeneza NARC muungano huo wa NARC ulishinda uchaguzi
huo na Mwai Kibaki alimteuwa waziri wa Afya Januari 3 2003.
Julai 31 2007 Ngilu alimpeleka Ann
Njogu mwandamaji hospitalini baada ya kupigwa na polisi, kisha
alihutumiwa na kukashifiwa kwa madai ya kumtorosha Njogu polisini,
alikamatwa na kufungwa Agosti 12 na kisha kutoka kwa thamani.
Oktoba 5,2007 ngilu alitangaza kujiunga
na ODM na mwaniaji urais wa chama hicho Raila Odinga katika kura za
2007 na alimlinganisha Bw Odinga na Bw Nelson Mandela.
Bwanake Micheal Mwendwa Ngilu aliaga
Julai mosi, 2006 Afrika Kusini na ana watoto watatu.
No comments:
Post a Comment