Pages

Thursday, 8 March 2012

BENJAMIN MKAPA

Mkapa alizaliwa mwaka wa 1938 huko Ndanda Tnzania kusini. Alihitimu kutoka Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda mwaka 1962 na shahada ya Kiingereza. Pia alihudhuria Chuo Kikuu cha Columbia mwaka 1963 na akatuzwa shahada yake katika masuala ya kimataifa.
Alikuwa ni afisa wa utawala wa Dodoma na waziri wa Teknolojia ya Sayansi na Elimu ya juu.
Tangu mwaka 1977 hadi 1990 alikuwa ni Waziri wa mambo ya kigeni.
Katika mwaka wa 1995, Mkapa alichaguliwa kuwa rais wa Tamzania kwa kufuatilia misingi ya kampeni maarufu ya kupambana na rushwa na kuwa mfuasi mwamini wa aliyekuwa rais wa Tanzania Julius Nyerere.
Mkapa alitoa juhudi za kupambana na rushwa na kuumba jukwaa la wazi la Rushwa la Tume ya Rais.
Akiwa bado rais, Mkapa alibinafsisha mashirika ya serikali na akaweka sera za soko huru,
Wafuasi wake walisema kuwa kuvutia uwekezaji wa kigeni ungesaidia kukuza uchumi.
Sera zake zilipata msaada wa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani na kusababisha kufutwa kwa baadhi ya madeni ya kigeni ya Tanzania.
Uongozi wake kama rais wa Tanzania ulifika kikomo mwezi Desemba mwaka 2005.

No comments:

Post a Comment