Pages

Friday, 9 March 2012

TIRUNESH DIBABA



Dibaba

Pia anajulikana kama Tirunesh Dibaba Kenene alizaliwa Oktoba 1 1985 huko Bekoji, Arsi Uhabeshini (Ethiopia). Ni mwanariadha wa masafa marefu. Kwa sasa Ndiye bingwa wa Olompiki kwa mbio za mita 5000 na mita 10,000, amepewa jina la utani 'Baby Faced Destroyer'.

Alizaliwa katika kijiji cha Bekoji, Dibaba ni mtoto wa 4 kwa watoto 6. Alianza riadha akiwa na umri wa miaka 14, na alihamia mji mkuu wa Addis Ababa mwaka 2000.

Dibaba anatoka kwa familia ya wanariadha dada zake na ndugu zake pia wakiwa kwenye nyanja hiyo ya riadha.
Dibaba amepata mafanikio makubwa katika michuano ya dunia matukio ya riadha ya 2003,2006 na 2007.
Aliweka upya rekodi ya dunia katika mbio za mita 5000 kwa muda wa 14:11.15 katika mkutano wa Oslo Golden League mwaka 2008.
Alishinda dhahabu kwa mbio za mita 10,000 katika michezo ya Olimpiki huko Beijing Agosti 2008, na kuweka rekodi mpya ya Olimpiki kwa muda wa 29:54.66 rekodi ya hapo awali ikishikiliwa na binamuye Deratu Tulu kwa muda wa 30:17.49 katika michezo ya Summer Olimpik huko Sydney 2000.

Wiki moja baadaye akashinda mbio za mita 5000 Agosti 22 2008.
Dibaba ameolewa kwa mshindi wa mbio za Olimpiki wa mwaka wa 2004 na 2008 Sileshi Sihine.

No comments:

Post a Comment