Pages

Thursday, 15 March 2012

GRACE OGOT



Ni mwandishi, Nesi, Mwandishi wa habari, Mwanasiasa na Mwanadiplomasia kutoka Kenya.
Alipozaliwa alipewa jina la Grace Emily Akinyi katika sehemu wilayani Asembo, katika mkoa wa Nyanza. Alisomea mafunzo yake ya nesi nchini Uganda na Uingereza. Alifanya kazi kama mkunga, kama mwalimu, kama mwandishi wa habari, kama mtangazaji wa huduma ya ng'ambo ya BBC, na katika cheo cha usimamizi katika kampuni ya Air India Corporation ya Afrika Mashariki. Mwaka wa 1984 akawa moja wa wanawake wachache kuhudumu kama mbunge na mwanamke wa kipekee aliyehudumu ka naibu Waziri katika Baraza la Mawaziri la Rais Daniel arap Moi.

Tangu wakati huo ameshikilia nyadhifa mbalimbali za ubalozi kwani amewakilisha nchi yake katika Umoja wa Mataifa na UNESCO. Alikuwa mwanachama mwanzilishi wa shirika la Waandishi wa Kenya maarufu kwa Kiingereza kama Writers' Association of Kenya.

Grace Ogot aliyezaliwa 1934 alifunga ndoa na mwanahistoria Profesa Bethwell Allan Ogot, kutoka sehemu ya Gem, mnamo mwaka wa 1959 na ni mama wa watoto wanne.
Kitabu chake cha kwanza kilikuwa Land Without Thunder kitabu cha hadithi fupi. Riwaya yake ya kwanza ilikuwa The Promised Land.

Grace Ogot anaweza kusemekana kuwa mmoja ya waandishi bora zaidi barani Afrika. Mtindo wake wa uandishi wake ni wa kuvutia sana hasa katika ubunifu wake wa wazi; yeye huweza kuonyesha Utabibu wa mila na tamaduni ya Kiafrika, yanayofuata njia mwafaka na ishara.

No comments:

Post a Comment