David
Lekuta Rudisha alizaliwa Decemba 17 1988 ni mkimbiaji wa Kenya na ana
rekodi ya dunia katika mbio za mita 800 kwa muda wa 1:41.01. Rudisha
pia anashikilia rekodi nne za mbio kumi bora ulimwenguni.
Kazaliwa
katika Kovai Wilaya ya Transs Mara, alipata elimu yake katika shule
ya upili ya Mtakatifu Francis Kimuron huko Iten Wilaya ya Keiyo,
ambayo pia imekuza na kuwalea wakimbiaji kadhaa. Awali alikuwa
mkimbiaji wa mita 400 lakini kocha wake alimsababisha kujaribu mita
800.
Mwaka
wa 2006 akawa bingwa wa dunia katika kitengo cha junior cha umbali
huo.
Rudisha
alishiriki katika mbio za 2009 World friidrott, na kufikia mita 800
nusu fainali. Septemba 2009, Rudisha alishinda mbio za IAAF Grand
Prix huko Italia na kuweka rekodi mpya ya Afrika kwa muda wa 1:42.01.
na kuvunjilia mbali rekodi ya miaka 25 ya muda wa 1:42.28 iliyowekwa
na Sammy Koskei.Juhudi zake zikamweka katika nafasi ya nne katika
orodha ya muda wote. Katika mbio za IAAF Diamond League mwaka wa 2010
alishinda na kutupilia mbali rekodi ya hapo awali iliyokuwa
imeshikiliwa na Sebastian Coe kwa miaka 31 kwa muda wa 1:42.04 na
kumweka katika orodha nyingine ya watu kumi bora katika mbio za mita
800. Tarehe 10 July 2010, Rudisha alishiriki katika KBC Night of
Athletics huko Ubelgiji katika mbio za mita 800 na kuweka rekodi
nyingine mpya ya 1:41.51 na kumweka nambari mbili duniani kwenye mbio
hizo.
Rudisha
sasa anashikilia rekodi ya dunia kwenye mbio mita 800 alivunja rekodi
ya hapo awali iliyokuwa imewekwa mwka wa 2007 kwenye mbio za ISTAF
IAAF World Challenge huko Berlin Agosti 22 2010 kwa muda wa 1:41.09.
Rekodi ya hapo awali ikishikiliwa na mzaliwa wa Kenya lakini hivi
sasa ni raiya wa Denmark Wilson Kipketer. Rudisha alivunja rekodi
hiyo kwa sekunde 0.02.
Novemba
2010 akiwa na umri wa miaka 21 alikuwa mkimbiaji mchanga duniani
kuwahi kushinda tuzo la mkimbiaji bora Duniani la IAAF, alishinda
pia mwanaspoti bora wa mwaka Kenya.
Rudisha
ni mwanachama wa kabila la wamaasai, babake Daniel Rudisha mkimbiaji
mstaafu aliyeshinda nishani ya fedha katika mbio za Olympiki mwaka
1968 katika mbio za rely za 4 x400 wakati mamake ni mstaafu wa mbio
za mita 400.
Amemuowa
Lizzy Naanyu na wana binti mmoja.

No comments:
Post a Comment