Pages

Wednesday, 7 March 2012

David Rudisha



David Lekuta Rudisha alizaliwa Decemba 17 1988 ni mkimbiaji wa Kenya na ana rekodi ya dunia katika mbio za mita 800 kwa muda wa 1:41.01. Rudisha pia anashikilia rekodi nne za mbio kumi bora ulimwenguni.
Kazaliwa katika Kovai Wilaya ya Transs Mara, alipata elimu yake katika shule ya upili ya Mtakatifu Francis Kimuron huko Iten Wilaya ya Keiyo, ambayo pia imekuza na kuwalea wakimbiaji kadhaa. Awali alikuwa mkimbiaji wa mita 400 lakini kocha wake alimsababisha kujaribu mita 800.
Mwaka wa 2006 akawa bingwa wa dunia katika kitengo cha junior cha umbali huo.

Rudisha alishiriki katika mbio za 2009 World friidrott, na kufikia mita 800 nusu fainali. Septemba 2009, Rudisha alishinda mbio za IAAF Grand Prix huko Italia na kuweka rekodi mpya ya Afrika kwa muda wa 1:42.01. na kuvunjilia mbali rekodi ya miaka 25 ya muda wa 1:42.28 iliyowekwa na Sammy Koskei.Juhudi zake zikamweka katika nafasi ya nne katika orodha ya muda wote. Katika mbio za IAAF Diamond League mwaka wa 2010 alishinda na kutupilia mbali rekodi ya hapo awali iliyokuwa imeshikiliwa na Sebastian Coe kwa miaka 31 kwa muda wa 1:42.04 na kumweka katika orodha nyingine ya watu kumi bora katika mbio za mita 800. Tarehe 10 July 2010, Rudisha alishiriki katika KBC Night of Athletics huko Ubelgiji katika mbio za mita 800 na kuweka rekodi nyingine mpya ya 1:41.51 na kumweka nambari mbili duniani kwenye mbio hizo.

Rudisha sasa anashikilia rekodi ya dunia kwenye mbio mita 800 alivunja rekodi ya hapo awali iliyokuwa imewekwa mwka wa 2007 kwenye mbio za ISTAF IAAF World Challenge huko Berlin Agosti 22 2010 kwa muda wa 1:41.09. Rekodi ya hapo awali ikishikiliwa na mzaliwa wa Kenya lakini hivi sasa ni raiya wa Denmark Wilson Kipketer. Rudisha alivunja rekodi hiyo kwa sekunde 0.02.
Novemba 2010 akiwa na umri wa miaka 21 alikuwa mkimbiaji mchanga duniani kuwahi kushinda tuzo la mkimbiaji bora Duniani la IAAF, alishinda pia mwanaspoti bora wa mwaka Kenya.
Rudisha ni mwanachama wa kabila la wamaasai, babake Daniel Rudisha mkimbiaji mstaafu aliyeshinda nishani ya fedha katika mbio za Olympiki mwaka 1968 katika mbio za rely za 4 x400 wakati mamake ni mstaafu wa mbio za mita 400.

Amemuowa Lizzy Naanyu na wana binti mmoja.

No comments:

Post a Comment