Martha Wangari Karua alizaliwa 22 Septemba 1957, ni mwanasiasa kutoka Kenya na pia ni mbunge wa Gichugu na wakili wa mahakama kuu ya Kenya. Alikuwa waziri wa Sheria lakini alijiuzuli mnamo Aprili 2009.

Alifanya kazi
katika mahakama ya hakimu wilayani na kupanda ngazi hadi Hakimu mkazi
Mwandamizi hadi alipotoka 1987. Katika kipindi hiki, alikuwa alikuwa
msimamizi wa mahakama za sheria Makadara 1984 – 1985 na Mahakama za
Kibera 1986 – 1987.
Yeye alichangia
kwa kiasi kikubwa maendeleo ya sheria ya familia na hasa ugawaji wa
mali ya ndoa pamoja na sheria ya kikatiba na utawala.
Kutoka mwaka wa
1990 – 2002 alikuwa mwanachama wa harakati za upinzani wa kisiasa
ambao walipigania demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya katika miaka
ya 1990 wakati Kenya ilikuwa chini ya utawala wa Daniel Moi.
Alikuwa mmoja
wa waliotengeneza chama cha NARC kilichoshinda kura za 2003 na
kumaliza miongo minee ya utawala wa KANU.
Alichaguliwa
kuwa mwenyekiti wa NARC Novemba 15 2008.
Alikuwa waziri
wa kwanza kujiuzulu kwa hiyari yake tangu 2003.
No comments:
Post a Comment