Pages

Wednesday, 15 February 2012

ABEDI AYEW



Anajulikana kitaalamu kama Abedi Pele, alizaliwa Novemba 5 1964 alikuwa mchezaji wa zamani na nahodha wa Ghana. Alipata umaarafuru akichezea soka katika Ligue 1 ya Ufaransa na Lille OSC na Olypique Marseille. Alipewa jina la utani la ''Pele'' katika kutambua uwezo wake mkuu kulinanishwa na mchezaji wa Brazil Pele.

Abedi Pele alikuwa mmoja wa waanzilishi wa mpira wa miguu ya Afrika katika Ulaya. Ni mmoja wa wachezaji wa kwanza wa Afrika kuchezea soka kwenye vilabu vya Ulaya kama vile Uswisi, Ujerumani na pia Italia, ni maarufu huko Ufaransa alikochezea sana haswa kwenye kilabu cha Marseille katika Ligi ya Mabingwa Ulaya wakati wa miaka ya 1990.

Aliondika Ghana kwenda Qatar baada ya Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka wa 1982. Baada ya miaka michache alirudi Ghana na akakosa kusajiliwa na klabu ya Kotoko kisha baadaye alijiunga na kilabu ya AS Dragons FC de l'Oueme ya Benin. Alirudi Ghana na kujiunga na timu ya Real Tamale United kwa Muhula mmoja. Alianza soka yake ya kimaaifa huko Ufaransa na klabu ya Chamois Niort, Montpellier na Lille kisha akajiunga na Olympique Marseille, baadaye alihamia Lyon.

Alikuwa nahodha wa timu ya soka ya Ghana kwa miaka 6 tangu 1992 – 1998 na alikuwa mwafrika wa kwanza kumaliza katika nafasi ya kwanza ya mchezaji bora wa FIFA orodha ya mwaka 1991 na 1992. Ni mchezaji bora wa Afrika ameshinda tuzo kadha wa kadha zikiwemo Shirikisho la soka Afrika, Tuzo la mchezaji bora la BBC, alituzwa pia kuwa mchezaji bora katika kombe la mataifa la Afrika 1992 na aalikuwa man of the match katika fainali ya mechi ya kihistoria ya Ligi ya Mabingwa ya Ulaya kati ya Marseille na Milan mwaka 1993.

Ana mtoto ambaye pia alifuata nyayo zake na pia anachezea timu ya nyumbani ya Ghana na alikuwa miongoni mwa wachezaji waliokuwa kwenye Kombe la Afrika lililokamilika hapo jana.

Abedi Pele Ayew alizindua mnara wake huko Equitorial Guinea wakati wa michezo hiyo kwa kuwa mchezaji bora kuwahi tika barani Afrika.

No comments:

Post a Comment