Robert Gabriel Mugabe
amekuwa kiongozi wa Zimbabwe
tangu 1980.
Yeye ni mwenyekiti wa chama tawala cha ZANU.
1980 alikuwa waziri
mkuu na 1987 Rais
wa Zimbabwe. Kabla ya wakati
ule aliongoza upinzani wa ZANU dhidi ya serikali ya walowezi
Waingereza nchini waliofuata siasa ya ubaguzi wa rangi.
Mugabe alirudiwa katika uchaguzi
mbalimbali. Tangu mwaka 2000 uchaguzi hizi zimekuwa mashakani
kutokana na matishio na matumizi ya mabavu dhidi ya wapinzani.
Utawala wa Mugabe umeitwa wa kidikteta tangu mwaka 2002. Kutokana na
mashtaka dhidi ya serikali ya Mugabe ya kudharau haki za binadamu,
nchi ya Zimbabwe ilisimamishwa ndani ya Jumuiya
ya Madola. Mugabe pamoja na
mawaziri wake na viongozi wa chama chake hawaruhusiwi kusafiri kwenda
nchi za Umoja
wa Ulaya na Marekani.
Mwanzoni mwa utawala wake Mugabe
alisifiwa kujenga uchumi na sera ya elimu nchini. Zimbabwe ilikuwa
nchi iliyouza vyakula vingi nje. Tangu mwanzo wa milenia mpya pamoja
na mashtaki ya udikteta hali ya uchumi ulirudi nyuma. Takriban
milioni mbili ya raia wa Zimbabwe wameondoka nchini wakikaa kama
wakimbizi Afrika
Kusini.
Baada tu ya kushika madaraka, Mugabe
aliamua kuimarisha jeshi lake la kumlinda (liitwalo Gukurahundi)
ambalo lilijengwa na watu kutoka kabila lake la wa-Shona. Nchi hiyo
ilikuwa tayari imegawanyika kikabila hata katika uchaguzi wa kwanza
wa 1980, washona wote walimchagua Mugabe na Wa-Ndebele na wabunge
kutoka chama cha ZANU. Wakati wandebele walichagua viongozi kutoka
chama cha ZAPU kilichoongozwa na Joshua Nkomo.
Mara baada ya uchaguzi tu mwezi Novemba
1980 Mugabe alianza kampeni ya kuua kwa wingi watu wa kabila la
wa-Ndebele ambao mji wao mkubwa unaitwa Bulawayo. Ingawa mauaji hayo
hayakufikia kiwango cha yale ya Rwanda na Burundi, waliuawa wanawake,
wanaume, watoto na hata vichanga vilivyokuwa matumboni. Mwaka 1981
pia Mugabe aliendelea kuua wandebele tukio ambalo halikutangazwa sana
na vyombo vya habari. Kuanzia enzi hizo hadi leo raisi Mugabe
amejaribu kushinda kila uchaguzi unaokuja nchini huko kwa kutumia
nguvu za kikabila na mabavu.
Alizaliwa Februari 21,1924 katika Zvimba
Wilaya ya kaskazini magharibi ya Salisbury katika kusini mwa Rhodesia
kwa baba wa Malawi Gabriel Matibili na mama kutoka kwa kabila la
Shona wote wakatoliki. Yeye ni mtoto wa tatu kwa watotot sita.
Alikuwa na na ndugu wawili wakubwa, na mmoja wao, Micheal, alikuwa
maarufu sana katika Kijijini. Ndugu wote wawili waliaga dunia
alipokuwa mchanga na kumwacha na mdogo wake.Babake ambaye alikuwa
seremala aliiacha familia yake mwaka 1934 baada ya kifo cha Micheal
alipokuwa akitafuta kazi huko Bulawayo.
Mugabe alikuzwa katika mazingira ya
kikatoliki na kusomea vyuo vya kikatoliki kama Marist Brothers na
Jesuit. Kulingana na kakake Mugabe alikuwa mpole na rafiki wake
mkubwa alikuwa vitabu.
Alihitimu kama mwalimu lakini aliondoka
kwenda kusoma katika Fort Hare nchini Afrika Kusini alipokuwa huko
alikutana na Julius Nyerere, Herbert Chitempo na Keneth Kaunda. Kisha
alienda kusoma Salisbury 1953, Gwelo 1954, na Tanzania 1955-1957. Apo
awali alifuzu na Shahada ya Sanaa kutoka chuo kikuu cha Fort Hare
mwaka 1951. Mugabe hatimaye alipata digri zaidi ya sita akiwa
akisafiri ikiwa ni pamoja na Shahada ya Utawala na shahada ya Elimu
kutoka chuo kikuu cha Afrika Kusini na shahada ya Sayansi, shahada ya
sheria na zingine nyingi tu zote kutoka chuo kikuu cha London. Digri
ya sheria alipata alipokuwa gerezani nayo shahada ya uzamili ya
sayansi ya chuma alipata akiwa waziri mkuu.
Baada ya kufuzu, Mugabe alifunza katika
Chuo cha Mafunzo cha Chalimbana kilichoko Zambia toka 1955-1958,
baada ya hapo amefundisha katika Apowa shule ya Sekondari katika
Takoradi,katika mkoa wa magharibi mwa Ghana huko ndiko alikutana na
Sally Hayfron ambaye walifunga ndoa mwezi wa Aprili 1961
Mugabe alirudi Kusini mwa Rhodesia na
kujiunga na National Democratic Party{NDP} mwaka 1960 wakati wa
utawala wa waziri mkuu Ian Smith. Mwaka 1980 Machi 4 Mugabe alishinda
kura na kuwa waziri mkuu licha ya kutokana vitisho kutoka pande zote,
kutoaminiana kutoka kwa vikosi vya usalama na kupata ripoti ya
masanduku ya kura kupatikana kwenye barabara.
Mwaka 1987, nafasi ya Waziri mkuu
ilifutiliwa mbalina Mugabe na kuwa Rais mtendaji wa Zimbabwe na
kupata nguvu zaidi. Alichaguliwa tena mwaka 1990 na 1996 na mwaka
2002 huku kukiwa na madai ya kuenea kwa wizi wa kura na vitisho
Katika kiaka ya 1980 sera ya Mugabe ya
Ujamaa ilionekana kukuza nchi hiyo, mwaka 1980 na 1981 uchumi wa
Zimbabwe ulikuwa kwa asilimia 10.65 na 12.5% kutoka asilimia 2.7%.
Kutokana na ripoti hiyo kwa mujibu wa Benki ya Dunia 1995 baada ya
uhuru Zimbabwe ilitoa kipaumbele katika uwezekaji wa rasilimali na
msaada kwa ajili ya kilimo cha wakulima wadogo wadogo.
Hata hivyo jamaa huyu ameshtumiwa kwa na
mtazamo wa ubaguzi wa rangi kwa wazungu, pia jamaa huyu amekuwa
suluhu katika upinzani wake kwa haki za ushoga.
Uchaguzi ujao ulikuwa ufanyike 2013,
lakini umepelekwa mbele hadi 2012 kwa madai kwamba umri wake ni
mkubwa licha ya hayo chama chake cha ZANU-PF kimesema kwamba bado
atawania urais.
Kwa sasa yeye ndiye rais aliyehudumu kwa
mda mrefu barani afrika, mwaka wa 2005 alipelekwa hospitalini kwa
kuwa na mshtuko wa moyo jambo ambalo lilipeleka uvumi kwamba
amefariki.
Mke wake wa kwanza Sally Hayfron aliaga
dunia 1992 kwa shida ya figo mtoto wao wa pekee kijana Micheal
Nhamodzenyika Mugabe aliyezaliwa septemba 27 1963 pia aliaga Desemba
26 1966 kutokana kutokana na malaria ya ubongo. Sally ambaye alikuwa
pia mshauri mkuu wake wa kisiasa inasemekana kwamba baada ya kifo
chake Mugabe alianza kuiongoza Zimbabwe vibaya.
Agosti 17 1996 alimuowa aliyekuwa karani
wake Grace Marufu ambaye ni mchanga wake kwa miaka41 na wana watoto
wawili naye, yeye tayari alikuwa na mimba ya Mugabe akiwa bado ana
mke wake wa kwanza Sally na wakati huo Grace alikuwa kwenye ndoa yake
na Stanley Goreraza, sasa mwanadiplomasia nchini Chini.Sasa wana
watoto watatu naye.
USICHOJUA KUMHUSU
Anapoadhimisha miaka 88 leo anajulikana
sana kwa kutumia pesa za watozwa ushuru kuadhimisha sherehe hizi.
Ndiye rais aliyesoma na ana shahada zaidi
ya 16 ulimwenguni
Alifungwa jela miaka 10 kuanzia 1964 kwa
kupinga utawala wa wakoloni.
Ndiye rais aliyeongoza kwa mda mrefu
barani afrika.
No comments:
Post a Comment