Alizaliwa
kama Albert Roger Miller Mooh tarehe 20 Mei 1952 ni mwanasoka mstaafu
kutoka Cameroon aliyecheza kama Mshambuliaji. Alikuwa mwafrika wa
kwanza ambaye Nyota yake iling'aa katika kandanda kimataifa.
Alichezea timu yake ya Camerron mara tatu kwenye Kombe la Dunia.
Alipata
mafanikio mengi akiwa na kiaka 38 umri ambao washambulizi wengi
hustaafu wakifika. Alifunga mabao manne kwenye Kombe la Dunia
mwaka1990, bao lililompa umaarufu na kumfanywa kukumbukwa ni lile
wakicheza na Colombia ambapo alionyesha ujuzi na mahanjam yake na
kumchenga kipa Rene Higuitana kufunga katika yadi 35 kutoka lango
lake na kusaidia Cameroon kufika robo fainali ikawa timu ya kwanza
kutoka Afrika kifikia kiwango hicho.
Pia
anakumbukwa kwa ishara yake ya kusherehekea bao alipofunga, kwa
kukimbia hadi kwenye kibendera cha kona na kuanza kucheza ngoma.
Pele
wa Brazil alimtaja miongoni mwa wachezaji 125 waliosifika kwenye
mchezo huo ambao bado wanaishi.
Alizaliwa
katika mji mkuu wa Yaounde'. Alianza kucheza soka akiwa na miaka 13
kwenye klabu ya Douala na akiwa na miaka 18 alishinda ligi yake ya
kwanza. Mwaka wa 1974 alipewa tuzo la mchezaji bora wa Afrika. Mwaka
wa 1977 alihamia ulaya na kuchezea klabu ya Valenciennes huko
Ufaransa, hata hivyo aliwekwa kwenye timu ya hifadhi miaka miwili.
Mwaka wa 1979 alijiunga na AS Monaco lakini bado akajipata palepale
kwenye hifadhi,mwaka uliofuatia alijiunga na klabu ya Bastia lakini
bado hakustawi, hatimaye akapata umaarufu kwenye klabu ya
Saint-Etienne mwaka 1984.
Alichezea
timu yake ya Cameroon mara ya kwanza mwaka wa 1978, alikuwa pia
miongoni mwa wachezaji wa timu hiyo waliocheza Kombe la Dunia mwaka
wa 1982, na bao lake lilikataliwa wakicheza dhidi ya Peru. Miaka
miwili baadaye alikuwa katika kikosi cha mashindano ya Michezo ya
Olimpiki ya 1984 huko Los Angeles ,California. Alistaafu kutoka soka
ya kimataifa mwaka 1987 na kuhamia Reunion katrika Bahari ya Hindi.
Hata
hivyo, mwaka 1990, alipokea simu kutoka kwa Rais wa Cameroon wakati
ule Paul Biya ambaye alimsihi na kumbembeleza kutoka ustaafuni na
kujiunga tena na timu taifa. Alikubali na kwenda Italia na
Indomitable Lions kucheza Kombe la Dunia 1990.
Alijitokeza
kama mchezaji kama mchezaji mashuhuri kwenye Kombe hilo kwa kufunga
mabao manne, mawili kwenye muda wa nyongeza na pia jinsi alivyo
yasherehekea mabao hayo yote manne.
Bao
lake la pili dhidi ya Colombia mwaka huo ndilo lililokuwa mada kwenye
Kombe la Dunia 2010 na kuwa kwenye matangazo ya Coca Cola.
Mwaka
wa 1994 alirudi tena kucheza kwenye Kombe la Dunia akiwa na umri wa
42, na kuwa mchezaji mkongwe kucheza kwenye Kombe la Dunia, Cameroon
wakabwagwa nje katika hatua ya makundi lakini kama kawa Milla
alifunga bao dhidi ya Urusi na kuweka redi kama mfungaji mkongwe
kwenye dimba hilo.
Kutokana
na umaarufu wake Pepe Kalle alimwimbia wimbo.
No comments:
Post a Comment