Pages

Wednesday, 8 February 2012

DESMOND TUTU



Alizaliwa Oktoba 7 1931 ni mwanaharakati wa Afrika Kusini na Askofu mstaafu ambaye alipata umaarufu kote duniani katika miaka ya 1980 kama mpinzani wa ubaguzi wa rangi. Alikuwa mwafrika mweusi wa kwanza huko Cape Town.

Tutu amefanya kazi katika ulinzi wa haki za binadamu na anatumia wasifu wake kwa kufanya kampeni ya ugandamizaji haki za binadamu. Amefanya kampeni za Ukimwi, Kifua Kikuu, Ubaguzi wa Rangi, na Umaskini.

Tutu alipata tuzo la Nobel mwaka 1984 na pia ameandika vitabu kuhusu hotuba zake na maneno yake,

Desmond Tutu Mpilo I mtoto wa pili kati ya watatu wa mzee Zacheriah.
Tutu alisomea katika chuo cha Pretoria Bantu Normal kwanzia 1951 – 1953 na kwenda kufundisha katika shule ya Johannesburg kisha aliendelea na masomo yake na kusomea theolojia katika chuo cha Theolojia ya Mtakatifu Petro katika Rosettenville.

Kisha alisafiri hadi Chuo Cha Mfalme wa London 1962 – 1966 ambapo alipokea shahada yake na shahada ya mwalimu katika Theolojia.

Dec 2 July 1955 Tutu alifunga ndoa na Nomalizo Leah Shenxane mwalimu ambaye walikutana Chuoni.Walibarikiwa na watoto wanne.
Mwaka wa 1989 mtoto wake mmoja Trevor Tutu alisababisha uwoga wa bomu katika Uwanja wa Ndege wa East London na alikamatwa.
Naomi Tutu alifuata nyayo za babake na kuanzisha Foundation kwa ajili ya Maendeleo na Misaada ya Kusini mwa Afrika mjini Hartford na pia ni mwanaharakati wa haki za binadamu.Bintiye mwingine Mpho Tutu pia alifuata nyayo za babake na yeye ni mwanzilishi na mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Tutu kwa ajili ya Sala na mwenyekiti wa bodi ya Muungano wa ukimwi.

Mwaka wa 1997 Tutu alishikwa na saratani ya kibofu na lifanyiwa matibabu huko marekani kwa mafanikio.

Tutu alikuwa askofu wa Lesotho kuanzia mwaka 1976 – 1978 kisha akawa katibu mkuu wa Afrika Kusini Baraza la Makanisa.

Wakati katiba mpya ilipendekezwa kwa ajili ya Afrika Kusini mwaka 1983 na kuilinda dhidi ya harakati za kupambana na ubaguzi wa rangi, Tutu alisaidia kwa kuunda Taifa Forum kamati ya kupambana na mabadilikoya katiba.

Mwaka wa 1993 aliteuliwa kuwa mlinzi wa kamati ya Olompiki ya Cape Town. Mwaka 1994 aliteuliwa mlinzi wa kampeni ya Dunia dhidi ya ushirikiano wa jeshi la Nuclear na Afrika Kusini

Alistaafu kama Askofu Mkuu wa Cape Town mwaka 1996 na akawa emeritus Askofu Mkuu wa cape Town.Tangu kustaafu kwake amefanya kazi kama mwanaharakati wa kimataifa katika masuala yanayohusu Uhuru, Demokrasia na haki za binadamu.

Alisema yeye husoma bibilia kila siku na inampenza akisikia kwamba watu husoma kitabu hicho.

No comments:

Post a Comment