Alizaliwa Oktoba 7 1931 ni
mwanaharakati wa Afrika Kusini na Askofu mstaafu ambaye alipata
umaarufu kote duniani katika miaka ya 1980 kama mpinzani wa ubaguzi
wa rangi. Alikuwa mwafrika mweusi wa kwanza huko Cape Town.
Tutu amefanya kazi katika ulinzi wa
haki za binadamu na anatumia wasifu wake kwa kufanya kampeni ya
ugandamizaji haki za binadamu. Amefanya kampeni za Ukimwi, Kifua
Kikuu, Ubaguzi wa Rangi, na Umaskini.
Tutu alipata tuzo la Nobel mwaka 1984
na pia ameandika vitabu kuhusu hotuba zake na maneno yake,
Desmond Tutu Mpilo I mtoto wa pili kati
ya watatu wa mzee Zacheriah.
Tutu alisomea katika chuo cha Pretoria
Bantu Normal kwanzia 1951 – 1953 na kwenda kufundisha katika shule
ya Johannesburg kisha aliendelea na masomo yake na kusomea theolojia
katika chuo cha Theolojia ya Mtakatifu Petro katika Rosettenville.
Kisha alisafiri hadi Chuo Cha Mfalme
wa London 1962 – 1966 ambapo alipokea shahada yake na shahada ya
mwalimu katika Theolojia.
Dec 2 July 1955 Tutu alifunga ndoa na
Nomalizo Leah Shenxane mwalimu ambaye walikutana Chuoni.Walibarikiwa
na watoto wanne.
Mwaka wa 1989 mtoto wake mmoja Trevor
Tutu alisababisha uwoga wa bomu katika Uwanja wa Ndege wa East
London na alikamatwa.
Naomi Tutu alifuata nyayo za babake na
kuanzisha Foundation kwa ajili ya Maendeleo na Misaada ya Kusini mwa
Afrika mjini Hartford na pia ni mwanaharakati wa haki za
binadamu.Bintiye mwingine Mpho Tutu pia alifuata nyayo za babake na
yeye ni mwanzilishi na mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Tutu kwa
ajili ya Sala na mwenyekiti wa bodi ya Muungano wa ukimwi.
Mwaka wa 1997 Tutu alishikwa na
saratani ya kibofu na lifanyiwa matibabu huko marekani kwa mafanikio.
Tutu alikuwa askofu wa Lesotho kuanzia
mwaka 1976 – 1978 kisha akawa katibu mkuu wa Afrika Kusini Baraza
la Makanisa.
Wakati katiba mpya ilipendekezwa kwa
ajili ya Afrika Kusini mwaka 1983 na kuilinda dhidi ya harakati za
kupambana na ubaguzi wa rangi, Tutu alisaidia kwa kuunda Taifa Forum
kamati ya kupambana na mabadilikoya katiba.
Mwaka wa 1993 aliteuliwa kuwa mlinzi wa
kamati ya Olompiki ya Cape Town. Mwaka 1994 aliteuliwa mlinzi wa
kampeni ya Dunia dhidi ya ushirikiano wa jeshi la Nuclear na Afrika
Kusini
Alistaafu kama Askofu Mkuu wa Cape Town
mwaka 1996 na akawa emeritus Askofu Mkuu wa cape Town.Tangu kustaafu
kwake amefanya kazi kama mwanaharakati wa kimataifa katika masuala
yanayohusu Uhuru, Demokrasia na haki za binadamu.
Alisema yeye husoma bibilia kila siku
na inampenza akisikia kwamba watu husoma kitabu hicho.
No comments:
Post a Comment