Alizaliwa Agosti 16 1963 huko Mfululira.Anajulikana sana kwa
urahisi kama Kalusha. Alikuwa kocha wa Zambia na pia mwanakandanda,
ni mchezaji wa Zambia aliye imarika zaidi katika soka na mfungaji
bora zaidi na anajulikana kama mchezaji maarufu kuwahi kucheza soka
nchini Zambia. Alitajwa kama mchezaji bora wa mwaka kutoka Afrika
1988 na gazeti la France Football na kuorodheshwa miongoni mwa
wachezaji bora duniani na FIFA mwaka wa 1996 kisha kuchaguliwa na
akawa nambari 14 wachezaji bora wa dunia.
Alianza
kujishughulisha na soka utotoni mwake kama vijana wengine wa
Kiafrika, yeye na marafiki wake walicheza huko mitaani na hapo ndipo
aliaanza kupata ujuzi kwenye mchezo huo. Walikuwa wakicheza miguu
mitupu kwa mpira uliotengenezwa kwa makaratasi.Kila mara walikuwa
wakicheza na ndugu ya ambapo karibu kila mara walishinda.
Kalusha
aliona mechi nyingi sana akiwa bado na umri mdogo, akiwa na umri wa
miaka14 alikuwa tayari kashaanza kucheza mechi za Ligi na klabu ya
Blackpool.Bwalya alikuwa mjumbe wa kikosi cha kitaifa ambacho
walishiriki katika Michezo ya Olimpiki ya 1988 na kuweka alama yake
kwa kufunga mabao matatu katika ushindi wa 4 – 0 dhidi ya Italia.
Ingawa
alikuwa nahodha wa timu ya taifa ya kandanda wakati wa mechi za
kufuzu kwa Kombe la Dunia 1994, Kalusha hakuwa kwenye ndege ya
iliyoanguka Aprili27 1993 wakati timu nzima na wasimamizi wa soka
walifariki wakati ndege hiyo ilianguka kwenye bahari ya Atlantic
kwenye ufuo wa Gabon. Kisha alianza kutafuta na kutengeneza timu
nyingine ya taifa
Yeye
ndiye alikuwa mchezaji-kocha wakati wa mechi za kufuzu kombe la
dunia mwaka 2006. Tarehe 5 septemba 2004, Zambia ilicheza na Liberia,
na mechi ilikuwa sare bin sare, Kalu alivyokuwa akijulikana wakati
ule mwenye umri wa miaka 41, aliingia kwenye kipindi cha pili na
ilikuwa mechi yake ya 147na kufunga bao lake la 100, akasema amefunga
bao hilo kwa ajili ya Nchi yake. Hata hivyo, Zambia ilikuwa ya tatu
kwenye kundi hilo na kushindwa kufuzu kwa Kombe la Dunia Mwaka 2006.
Tunavyozungumza sasa hivi yeye ndiye msimamizi wa soka nchini humo na
alikuwepo Zambia ikishinda Kombe la Bara Afrika tarehe 12 Januari
2012.
Viva Zambia
ReplyDelete