Pages

Monday, 13 February 2012

KALUSHA BWALYA


 Alizaliwa Agosti 16 1963 huko Mfululira.Anajulikana sana kwa urahisi kama Kalusha. Alikuwa kocha wa Zambia na pia mwanakandanda, ni mchezaji wa Zambia aliye imarika zaidi katika soka na mfungaji bora zaidi na anajulikana kama mchezaji maarufu kuwahi kucheza soka nchini Zambia. Alitajwa kama mchezaji bora wa mwaka kutoka Afrika 1988 na gazeti la France Football na kuorodheshwa miongoni mwa wachezaji bora duniani na FIFA mwaka wa 1996 kisha kuchaguliwa na akawa nambari 14 wachezaji bora wa dunia.

Alianza kujishughulisha na soka utotoni mwake kama vijana wengine wa Kiafrika, yeye na marafiki wake walicheza huko mitaani na hapo ndipo aliaanza kupata ujuzi kwenye mchezo huo. Walikuwa wakicheza miguu mitupu kwa mpira uliotengenezwa kwa makaratasi.Kila mara walikuwa wakicheza na ndugu ya ambapo karibu kila mara walishinda.

Kalusha aliona mechi nyingi sana akiwa bado na umri mdogo, akiwa na umri wa miaka14 alikuwa tayari kashaanza kucheza mechi za Ligi na klabu ya Blackpool.Bwalya alikuwa mjumbe wa kikosi cha kitaifa ambacho walishiriki katika Michezo ya Olimpiki ya 1988 na kuweka alama yake kwa kufunga mabao matatu katika ushindi wa 4 – 0 dhidi ya Italia.

Ingawa alikuwa nahodha wa timu ya taifa ya kandanda wakati wa mechi za kufuzu kwa Kombe la Dunia 1994, Kalusha hakuwa kwenye ndege ya iliyoanguka Aprili27 1993 wakati timu nzima na wasimamizi wa soka walifariki wakati ndege hiyo ilianguka kwenye bahari ya Atlantic kwenye ufuo wa Gabon. Kisha alianza kutafuta na kutengeneza timu nyingine ya taifa

Yeye ndiye alikuwa mchezaji-kocha wakati wa mechi za kufuzu kombe la dunia mwaka 2006. Tarehe 5 septemba 2004, Zambia ilicheza na Liberia, na mechi ilikuwa sare bin sare, Kalu alivyokuwa akijulikana wakati ule mwenye umri wa miaka 41, aliingia kwenye kipindi cha pili na ilikuwa mechi yake ya 147na kufunga bao lake la 100, akasema amefunga bao hilo kwa ajili ya Nchi yake. Hata hivyo, Zambia ilikuwa ya tatu kwenye kundi hilo na kushindwa kufuzu kwa Kombe la Dunia Mwaka 2006. Tunavyozungumza sasa hivi yeye ndiye msimamizi wa soka nchini humo na alikuwepo Zambia ikishinda Kombe la Bara Afrika tarehe 12 Januari 2012.

1 comment: