Akinwande
Oluwole au "Wole"
Soyinka
ni mwandishi Mnageria .Wengi wanamwona kama mwandishi bora wa michezo
ya kuigiziwa Afrika.
Ni mwandishi na mtungi wa Mashairi na pia michezo ya kuigiza.
Alizaliwa
tar. Julai
13,
1934
kwa wazazi Wayoruba huko Abeokuta, Nigeria.
Alisoma shule ya msingi kwao Abeokuta halafu shule ya sekondari ya
Ibadan,kisha akasomea fasihi
kwenye Chuohicho cha Ibadan
(1952-1954) na Leeds
(Uingereza)
1954-1957.
Soyinka
aligongana mara nyingi na serikali za kidikteta za nchi yake akipinga
pia udikteta katika nchi mbalimbali kama vile utawala wa Mugabe
huko Zimbabwe.
Hasa
wakati wa udikteta
wa jenerali Sami
Abacha
(1993-1998) Soyinka alijikuta hatarini. Akaondoka Nigeria akaishi nje
alipopata kuwa profesa wa fasihi kwenye Chuo
Kikuu cha Emory
(Atlanta
- Marekani).
Februari
6 2012 Soyinka alisema kwamba yuko miongoni mwa watu maarufu na
mashuhuri wanaolengwa kuuwawa na kundi la Boko Haram.
Baada
ya mwisho wa utawala wa kijeshi mwaka 1999 Soyinka alikubali nafasi
kwenye chuo kikuu cha Ife kwa masharti ya kwamba mwanajeshi mstaafu
hatakuwa kamwe chansela wa chuo kikuu kile.
Wole
Soyinka amemwoa mke wake Laide wana watoto wanne. Aliwahi kuwa na
watoto wawili kabla ya kuoa.
JE WAJUA
Mwaka
1994 aliteuliwa kuwa balozi wa nia njema kwa{UNESCO}Umoja wa Mataifa
la Elimu,Sayansi,na Utamaduni kwa ajili ya kukuza Utamaduni wa
Kiafrika, haki za binadamu, Uhuru wa Kujieleza, Vyombo vya habari na
mawasiliano.
Ameandika
zaidi ya michezo 20.
No comments:
Post a Comment