Pages

Monday, 27 February 2012

Kipchoge Keino


Kipchoge ("Kip") Keino ni Mwenyekiti wa Kamati ya Olimpiki ya Kenya na mkimbiaji aliyestaafu akiwa na ushindi wa medali za dhahabu mara mbili kwenye Mashindano ya Olimpiki. Alizaliwa Januari 17, 1940 huko Kipsamo, Wilaya ya Nandi, Kenya.Wazazi wake wote walifariki akiwa changa na kukuzwa na shanagazi.
Alianza kuonyesha ufundi wake wa kukimbia kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola huko Perth, Australia alipochukua nafasi ya kumi na moja. Kwenye Mashindano ya Olimpiki ya Majira ya Joto mwaka 1964 alimaliza wa tano kwenye mbio za mita 5000.
Agosti 27, 1965, Keino alivunja rekodi ya dunia ya mita 3000 kwa sekunde sita. Katika Mashindano ya Mataifa ya Afrika alishinda medali mbili za dhahabu kwa umbali wa mita 1500 na 5000. Baadaye alikuja kuvunja rekodi ya dunia iliyokuwa ikishikiliwa na Ron Clarke ya mita 5000 kwa kukimbia kwa muda wa 13:24:2.
JE WAJUA
Aliwahi cheza mchezo wa raga.
Alijiunga na Kenya Police baada ya skuli.

No comments:

Post a Comment