Alizaliwa 1 Aprili 1940 alikuwa mwanaharakati wa masuala
ya mazingira na haki za wanawake kutoka nchini Kenya.
Mwaka wa 2004 alikuwa mshindi wa Tuzo
ya Nobel ya Amani.
Yeye ni mwanamke Mwafrika wa kwanza kupokea tuzo hilo. Pia, aliwahi
kuwa mbunge wa Kenya na waziri msaidizi katika serikali ya Mwai
Kibaki kati ya Januari 2003 hadi Novemba 2005.
Katika
maandalizi ya uchaguzi
wa 2007 Maathai alisimama upande wa rais Kibaki lakini
hakuteuliwa na chama cha PNU
akagombea kwa chama cha Mazingira Green Party lakini hakurudi
bungeni.
Maathai
alihudhuria shule ya msingi ya Ihithe,akiwa na miaka kumi na moja
alisomea shule ya kikatoliki ya Mt. Cecilia huko Nyeri akiwa huko
alikisoma Kiingereza na kukielewa vyema kisha akabadili dini na kuwa
mkatoliki na kupata jina Mary Josphine alipomaliza masomo yake kule
alijiunga na shule ya upili ya wasichana ya kikatoliki ya Loreto
Convent, Limuru. Baada ya kuhitimu
sekondari, alienda ng’ambo kusoma bayologia nchini Ujerumani
na Marekani. Mwaka wa 1967,
alipata shahada ya kwanza ya bayologia
kutoka Chuo Kikuu cha Benedictine, Marekani. Aliendelea na masomo
yake katika Chuo Kikuu cha Pittsburg ambako alipata shahada ya pili.
Halafu alirudi Nairobi na kupata shahada ya udaktari kutoka Chuo
Kikuu cha Nairobi katika somo la udaktari wa wanyama. Kuanzia
mwaka wa 1977, Maathai alikuwa profesa msaidizi wa anatomia
ya wanyama huko Nairobi akiwa mwanamke wa kwanza kupata uprofesa
katika chuo kikuu cha Nairobi.
Baadhi
ya tuzo zake ni Tuzo ya Mwanamke wa Dunia (1983), Tuzo ya Goldman kwa
Mazingira (1991), Elder of the Burning
spear (2003) kutoka serikali ya Kenya,
Tuzo ya Nobel ya Amani (2004), na Legion
D’Honneur (2006) kutoka serikali ya
Ufaransa.
Mwaka
wa 1977, Maathai alianzisha shirika la Green
Belt Movement ambalo linajihusisha hasa na mazingira, haki za
raia na demokrasia.
Mwaka
wa 1971 alikuwa mwanamke wa kwanza eneo la Afrika Mashariki kupata
Ph.D
Mwaka
wa 1969, Wangari Muta (jina lake la kuzaliwa) alifunga ndoa na Mwangi
Maathai, mwanasiasa wa Kenya. Wana watoto watatu, Waweru, Wanjira na
Muta, lakini walitengana baadaye.
Maathai
na mume wake, Mwangi Mathai, walitengana mwaka 1977. Baada ya
kujitenga kwa muda mrefu, Mwangi alipeleka kesi kotini kutaka talaka
mwaka 1979. Mwangi alisema kwambaWangari alikuwa mwanamke mwenye
akili nyingi na kwamba alikuwa "hawawezi kumdhibiti".Jaji
alikata rufa kwa upande wa Mwangi na akawa ameshinda kesi hiyo. Muda
mfupi baada ya kesi, katika mahojiano na gazeti la Viva, Maathai
alisema kwamba hakimu yule hajui kazi yake ama alipata rushwa jambo
ambalo lilimfanya kushtakiwa na kufungwa kwa miezi sita.
Muda
mfupi baada ya talaka, mume wake wa zamani aliandika barua kupitia
wakili wake, na kudai kuwa Maathai kuacha jina lake lakini badala
yake alichagua kuongeza herufi "a" badala yake.
Oktoba
1989 Maathai alikuja kutambua kwamba serikali inataka kujanga jumba
la orofa 60 katika uwanja wa Uhuru Park na jumba hilo lilikuwa liwe
makao makuu ya chama cha KANU. Mpango huo ulikuwa pia kusimamisha
sanamu ya rais wake ule rais Moi.Maathai aliandika barua kukataa
mipango hiyo lakini zilipuuzwa na serikali na kuzidi wakamwiita
mwanamke mwenye kichaa.
Tarehe
12 Desemba, katika Uwanja wa Uhuru Park, katika hotuba ya kuadhimisha
uhuru wa Kenya , Rais Moi alimshauri Maathai kuwa mwanamke sahihi
katika utamaduni wa Afrika na kuwapa watu heshima na kuwa na utulivu.
Mwaka
wa 2004 alipata tuzo la Amani la Nobel na kuwa mwanamke wa kwanza
kutoka Afrika na mwanaharakati wa mazingira kupata tuzo hilo.
Wangari
Maathai alifariki kutokana na matatizo yanayotokana na saratani ya
ovary wakati alipokuwa akipokea matibabu katika hospitali ya Nairobi
tarehe 25 Septemba 2011.
No comments:
Post a Comment