Pages

Friday, 24 February 2012

Ngũgĩ wa Thiong'o


Alizaliwa Januari 5 1938, Kamirithu karibu na Limuru katika Kaunti ya Kiambu, alibatizwa James Ngugi.Ni mwandishi wa Kenya hapo zamani aliandika kwa Kiingereza lakini sasa anaandika kwa lugha ya Gikuyu. Kazi yake ni pamoja na Riwaya, Michezo, Hadithi fupi na Insha, pia yeye ni mwanzilishili na mhariri wa jarida la ligha ya Gikuyu, Mutiiri.

Alipata Elimu katika shule za Kamandura, Manguu na Kinyogori na kisha kuelekea katika shule ya Upili ya Alliance High School zote toka Kenya, baada ya hapo alizidisha masomo yake kwenye Chuo Kikuu cha Makerere huko Uganda na Chuo Kikuu cha Leeds huko Uiingereza.

Ngugi ni mpokeaji wa Udakitari za Heshima saba kutoka vyuo vikuu tofauti tofauti.
Riwaya yake ya kwanza Weep Not Child kilichochapishwa 1964, alikiandika akiwa Katika Chuo Kikuu cha Leeds huko Uiingereza, na kumfanya kuwa mwafrika wa kwanza kutoka Afrika Mashiriki kuchapisha katika Lugha ya Kiingereza.

Mwaka wa 1967 baada ya kuchapisha riwaya yake Agrain of Wheat aliwacha kuandika kwa Kiingereza akaacha pia Ukisto na kumfanya kubadilisha Jina lake James Ngungi hadi Ngugi wa Thiongo na akaanza kuandika katika asili yake ya Gikuyu na Kiswahili. Mwaka wa 1977alichapisha mchezo Ngaahika Ndeenda yani ( I will Marry When I want) ambacho kilimkasirisha makamu wa Rais wakiti ule Daniel Arap Moi alipoamuru kufungwa. Ali[pokuwa kizuizini katika gereza la Kamiti Maximum aliandika riwaya ya kwanza ya Kisasa katika Gikuyu Caitaani Mutharaba yaani (Devil on the Cross) kwenye karatasi gushi.
Baada ya kutoka kwake hakurejeshewa kazi yake kama profesa katika Chuo Kikuu cha Nairobi, na familia yake ilikuwa inasumbuliwa kutokana na maadishi yake kuhusu kukosekana kwa haki na serikali ya kidikteta hata hivyo kulazimika kuishi uhamishoni. Alirudi baada ya miaka 22 wakati Moi alitoka Ofisini.

Tarehe 8 Agosti 2004 Ngugi alirejea Kenya kama ziara ya kuzuru Afrika Mashariki.Agosti 11, majambazi waliingia nyumbani kwake na kudhulumiwa pamoja na mke wake, na kuiba fedha na kompyuta jambo ambalo lilimfanya arudi Marekani hadi sasa.

Amechapisha riwaya, michezo,na hadithi fupi zaidi ya 30.

No comments:

Post a Comment