Pages

Wednesday, 15 February 2012

WATOTO WA MGANGA

Nchini Zambia wanawake wawili waliokuwa wamekwenda kumwona daktari,lakini walipokuwa wakimsubiri daktari huyo walizungumzia matatizo yao.
Mmoja alisema," Natamani sana kupata mtoto kuliko kitu kingine duniani, lakini nadhani haitawezekana."
Wapili akajibu," Mie pia nilidhani kuwa haiwezekani lakini mambo yakabadilika ndiposa niko hapa. Natarajia kupata mtoto kwa miezi mitatu zijazo."
"Basi niambie ulifanya vipi," akajibu.
"Mimi nilimtembelea mganga wa kienyeji."
Wa kwanza akajibu," Nimefanya hivyo nikiwa na mume wangu mwanzoni mwa mwaka huu lakini haikunifaidi."
Mwanamke wa pili akaangua kicheko na kumnong'onezea mwenzake kuwa,"Basi dada siku nyingine ukimtembelea mganga huyo usiende na bwanako."

No comments:

Post a Comment